• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakulima wa parachichi Mafinga wapewa elimu

Imewekwa tarehe: September 17th, 2020

WAKULIMA wa parachichi katika mji wa Mafinga wilayani Mufindi mkoani Iringa, wamepatiwa elimu ya kilimo bora cha zao hilo ambalo hivi sasa lina soko kubwa ndani na nje ya nchi.

Elimu hiyo imetolewa na Kampuni ya Agrigrow Tanzania Ltd yenye makao makuu yake katika mji wa Morogoro ambayo wana lengo la kuleta mageuzi makubwa katika kilimo hapa nchini.

Akizungumza katika mafunzo hayo Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara, Wilson Mbwambo alisema kuwa lengo la kuendesha mafunzo hayo ni kuwapatia mbinu za kilimo hicho wakulima ili kuongeza uzalishaji ambao unakubalika katika soko la kimataifa.

Hata hivyo, aliwataka wakulima hao kuchagua mbegu bora hasa pale wanapotaka kuanzisha vitalu vya miche ya parachichi kwani hiyo ndiyo hatua muhimu itakayomfanya mkulima kupata faida kwa kile anachozalisha.

Katika hatua nyingine, aliongeza kuwa hivi sasa kampuni hiyo itahakikisha wanatoa elimu mara kwa mara sambamba na kuwapatia virutubishi asilia kutoka Agrigrow ambavyo vitawaongezea uzalishaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mji wa Mafinga, Saada Mwaruka alisema kuwa katika kuunga mkono uzalishaji wa parachichi hivi sasa wana eneo lenye ukubwa ekari 50 ambazo zitatumika kama shamba darasa kwa wakazi wa mji huo.

Nao baadhi ya wakulima walisema kuwa hivi sasa wanakabiliwa na changamoto ya kupata miche bora ya zao hilo, ambalo linawaongezea kipato kikubwa kutokana na kuwa na soko la uhakika.

Hata hivyo, waliomba elimu hiyo itolewe mara kwa mara pamoja na wataalamu kufika katika mashamba ili kuangalia namna wanavyohudumia mashamba yao ya parachichi.

Akizungumzia suala la mbegu na miche bora ya parachichi, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Gerald Kusaya alisema kuwa hivi sasa vituo vya utafiti wa kilimo katika mikoa hiyo, vimeshaanza kuuza miche ambayo ni bora na yenye kuongeza uzalishaji.

Mafunzo hayo ya kilimo bora cha parachichi, yaliyoandaliwa na Kampuni ya Agrigrow Tanzania Limited yenye makao makuu yake katika mji wa Morogoro, yaliweza kuwajengea uwezo wakulima katika kukabiliana na magonjwa na wadudu wasumbufu katika zao hilo na mbinu za kujikinga nao.

Hata hivyo, waliahidi kuendelea kutoa elimu hiyo kwa wakulima wa mikoa hiyo ya Nyanda za Juu Kusini ili kuweza kuona faida ya kilimo cha parachichi ambacho kitaongeza kipato kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Chanzo: HabariLeo

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.