• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi Dodoma wahimizwa kutunza Mazingira

Imewekwa tarehe: February 2nd, 2025

Na. Aisha Ibrahim, DODOMA

MKUU wa Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa taka ngumu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro, alisema kitengo kicho kimejipanga kikamilifu katika kuendelea kutekeleza shughuli mbalimbali za udhibiti na uondoshaji wa taka ili kuhakikisha Jiji la Dodoma linakuwa katika hali ya usafi na kuvutia.

Aliyasema hayo nje ya Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani la kupitia rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Akizungumzia kuhusu udhibiti wa taka ngumu, Dickson Kimaro, alisema kupitia bajeti iliyotengwa na halmashauri, kitengo hicho kinajiandaa na mchakato wa kununua mitambo maalum kwaajili ya kuchakata takataka na kuwepo kwa gari ili kukusanya na kupeleka eneo la dampo kuu la Chidaya. “Tunatarajia kwenda kununua mitambo ya kuchakata takataka, lakini kununua malori kwaajili ya uondoshaji wa taka ili kuondokana na mfumo wa ‘Collection Point’, bali kuchukua taka hizo na kupeleka dampo letu la Chidaya”, alisema Kimaro.

Aidha, aliongeza kuwa katika bajeti hiyo kutakuwa na ukusanyaji wa takwimu ya watumiaji na wazalishaji wa taka ili kubaini kiwango cha uzalishaji wa taka hizo ikiwa ni njia mojawapo ya kuboresha mfumo wa ukusanyaji na uondoshaji wa taka katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Tunakwenda kukusanya takwimu za watumiaji na wazalishaji wa taka, maeneo walipo na kiwango wanachozalisha kwa lengo la kuboresha mfumo wa ukusanyaji na uondoshaji wa taka katika jiji la Dodoma”, alisema Kimaro.

Nae, Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe, alisema wananchi wanatakiwa kutunza mazingira kwa kupanda miti ikiwa ni juhudi za kuunga mkono agenda ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya utumiaji wa nishati safi ya kupikia. “Katika kumuunga mkono mheshimwa Rais, katika adhima yake ya nishati safi tunahimizwa utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti” alisema Prof. Mwamfupe.

Ukusanyaji na uhifadhi wa taka katika maeneo maalum ni njia mojawapo ya kuhakikisha maeneo mbalimbali yanakuwa katika hali ya usafi, pia kusaidia kuondokana na magonjwa ya mlipuko yanayosababishwa na uchafuzi wa mazingira.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.