• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

Imewekwa tarehe: May 21st, 2025

Na. Aisha Ibrahim, MADUKANI

Wananchi wa Kata ya Madukani, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuboresha huduma za afya katika Zahanati ya Chikande na kuwahakikishia matibabu bora na karibu.

Zahanati hiyo imeboresha huduma mbalimbali zikiwemo vipimo vya maabara kama malaria, wingi wa damu, virusi vya UKIMWI na afya ya mama na mtoto ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma stahiki na elimu kuhusu lishe bora karibu na makazi yao. 

Akizungumza kuhusu uboreshaji wa huduma za afya, Edina Rungwa ambae ni muuguzi katika zahanati hiyo alieleza kuwa wanatoa kipaumbele haswa kwenye huduma ya afya ya mama na mtoto kwa kutoa elimu kuhusu lishe bora na njia za kufuata ili kuepuka magonjwa katika kipindi cha ujauzito na baada ya kujifungua. “Kuhusu huduma ya afya ya mama na mtoto, zahanati hii tunajitahidi kwa ukubwa kuhakikisha mama wajawazito wanapata elimu ya kutosha kuhusu lishe bora na njia sahihi za kufuata ili kuepuka magonjwa mbalimbali. Hivyo, kuimarisha afya ya mtoto awapo tumboni na baada ya kuzaliwa” alisema Rungwa.

Akiongelea elimu ya lishe, alisema kuwa ni nzuri kwa mama mjamzito. “Elimu hii inamsaidia mama kujifungua mtoto mwenye afya na nguvu za kutosha, hatokuwa na shida yoyote ya maradhi. Vilevile, atazaliwa akiwa na uzito ambao ni sahihi” aliongeza.

Kwa upande wake, Pendo Edward, ambae ni mkazi wa Kata ya Madukani, alieleza kuwa kupitia kliniki ya afya ya mama na mtoto, wajawazito wanapewa elimu ya kutosha kuhusu lishe bora. “Hapa tunafundishwa kuwa mama mjamzito anatakiwa kula vizuri, kupumzika kwa wakati, kufanya mazoezi madogo madogo, kuepuka kazi nzito na kuhudhuria kliniki mara kwa mara ili kujua maendeleo ya afya ya mama na mtoto aliyepo tumboni” alisema Edward.

Pia, alishukuru serikali kwa kuboresha huduma za afya katika zahanati hiyo, ikiwemo elimu ya lishe bora kwa mama na mtoto kwasababu inawasaidia kujua njia bora zakujikinga na maambukizi mbalimbali. “Tunashukuru kwa elimu hii kwasababu kwetu inatusaidia kujua ni namna gani tunaweza kutunza afya zetu hata siku ya kwenda kujifungua hatupati shida yoyote” alisema Edward.

Maboresho yaliyofanyika katika zahanati hiyo ni ukarabati wa vyumba vya madaktari, maabara na huduma ya mama na mtoto yakiwa yamesaidia kwa kiasi kikubwa wananchi kupata huduma bora.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma atoa pongezi kwa Madiwani

    May 25, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.