• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi Kata ya Mnadani watakiwa kutokomeza ukatili wa kijinsia

Imewekwa tarehe: May 28th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WANANCHI wa Kata ya Mnadani wametakiwa kutokomeza ukatili wa kijinsia ili kuunga mkono juhudi za Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kupambana na ukatili huo na kuwaletea maendeleo.

Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Viti maalum Jiji la Dodoma, Asma Karim alipokuwa akiongea na wananchi wa Kata ya Mnadani iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Karim alisema kuwa jukumu la kupinga aina zote za ukatili wa kijinsia ni la jamii nzima. “Ndugu zangu, Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan hawezi kuja kuingia katika nyumba zetu na kutokomeza ukatili wa kijinsia. Sisi ndiyo jukumu letu kufanya hivyo na kuhakikisha kwamba ukatili wa kijinsia unaisha katika jamii yetu. Wanawake ni wahanga wa ukatili wa kijinsia kutokana na hali za kiuchumi. Umefika wakati kina mama kujikwamua kiuchumi ikiwa ni moja ya mkakati wa kukabiliana na tatizo la ukatili wa kijinsia” alisema Karim.

Aliwataka wanawake kuwa mstari wa mbele katika kulijenga taifa. “Wanawake asili yetu ni uchapa kazi. Tunamuona rais wetu alivyo mchapa kazi, sisi tumuunge mkono kwa kufanya kazi na kuijenga nchi yetu. “Tukizembea na kumtegemea Mheshimiwa Rais pekee haiwezekani, tukimuachia mbunge pekee haiwezekani, tukiwaachia madiwani pekee haiwezekani. Sote kwa umoja wetu lazima tufanye kazi kwa pamoja ili kukuza uchumi wetu” alisema Karim.

Wakati huohuo, aliwataka wanawake kuwa mstari wa mbele katika malezi ya watoto. “Kina mama nendeni mkalee watoto wetu. Malezi bora ya watoto na uangalizi wa karibu ni msingi katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia. Malezi bora kwa watoto yatatuwezesha pia kupiga hatua ya maendeleo katika jamii kwa sababu juhudi zenu za uchumi hazitatoa matunda. Mtajenga nyumba, mtatajirika na ninyi mtakuwa zii kwa sababu hakuna kinachoendelea kutokana na kuharibika kutokana na ukatili wa kijinsia” alisema Karim.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Kata ya Mnadani, Farida Mbarouk aliipongeza serikali kwa kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo katika Kata ya Mnadani. “Serikali imefanya mambo makubwa sana kutujengea shule, vituo vya afya na mikopo ya asilimia 10 isiyo na riba inayotolewa na halmashauri ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM. Serikali imetujengea madarasa tisa na sasa shule mpya inajengwa. Utekelezaji huu utaongeza ufaulu kwa wanafunzi katika Kata ya Mnadani kwa sababu walimu wapo wa kutosha” alisema Mbarouk.

Alisema kuwa suala la ardhi lilikuwa changamoto kubwa. “Sasa ardhi inapimwa na watu wanamilikishwa viwanja. Suala la miundombinu ipo vizuri, barabara zinapitika muda wote. Maji yanapatikana kila siku” alisema Mbarouk.

Madiwani 14 wa Viti maalum wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wanafanya ziara katika kata 41 za jiji hilo kutoa elimu dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii na fursa za kiuchumi.







Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.