• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi waanza ujenzi sekondari ya Kata ya Chahwa jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: March 4th, 2025

Na. Nancy Kivuyo, CHAHWA

Mkutano wa hadhara wa wananchi wa Kata ya Chahwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamefanikiwa kuzindua utekelezaji wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari kwa nguvu zao wenyewe kwa lengo la kusogeza huduma hiyo karibu na wananchi.

Akizungumza na wananchi hao, Diwani wa Kata ya Chahwa, Sospeter Mazengo aliwapongeza wananchi kwa moyo wa utayari na michango katika kujenga shule ya sekondari itakayopunguza adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kupata huduma ya elimu. Baadhi ya wananchi walichanga pesa taslimu pamoja na vifaa vya ujenzi, alisema. 

“Watoto wetu wamekua wakiteseka kutembea umbali mrefu kutoka Chahwa hadi Ipala kusoma, ninaamini tutafanikiwa katika hili tuliloazimia kulifanya kama tutaanza kwa nguvu ya pamoja. Inawezekana baadae kupata wadau wakatusaidia kumalizia pale ambapo tutaishia” alisema Diwani Mazengo.

Sambamba na hilo, aliwasisitiza kuwa kupitia maazimio yao waliyojiwekea kufikia mwezi Januari, 2026 madarasa manne yawe yamekamilika na masomo yaanze rasmi.

Kwa upande wake Sarah Mwakyusa, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Kata ya Chahwa alisema “kata ni yetu, maendeleo ni kwa faida yetu pia, tuwekeze nguvu zetu kwasababu tunaamini kwa kufanya hivyo, serikali itatuona na kutusaidia. Tushiriki ipasavyo katika kuchangia ujenzi huu kwaajili ya maendeleo yetu”. 

Aidha, Godfrey Mtundu, Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chahwa alieleza kuwa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi imeendelea kutekelezwa kikamilifu katani hapa kupitia utekelezaji wa ujenzi wa miradi mbalimbali pamoja na uboreshaji wa huduma za kijamii. Alishukuru wananchi kwa jitihada hiyo ya kuunga mkono juhudi za serikali kupitia ujenzi wa shule. “Nawakaribisha wadau mbalimbali mjitokeze kutuunga mkono kwenye ujenzi, tujenge shule yetu kwasababu maendeleo haya ni kwa vizazi vyetu na vya baadae” alimalizia Mtundu.

Naye, John Mtundu alisema “tunasikia raha sana kufanya ujenzi kwaajili ya kuwa na taifa la wasomi la baadae, nitoe rai kwa wananchi wenzangu kuchangia. Mimi naahidi shilingi 50,000 na hapa natanguliza shilingi 20,000. Ninachoweza kusema ni kwamba shule hii itakuwa na manufaa makubwa sana hapa kwetu”.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.