• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi watakiwa kuacha kufanya bahati nasibu kupata haki isiyostahili

Imewekwa tarehe: October 18th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WANANCHI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuacha tabia ya kufanya bahati nasibu ya kupata haki isiyostahili baada ya kuwa malalamiko yao yamekwisha tatuliwa kwa mujibu wa taratibu na sheria.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi waliojitokeza kutatuliwa kero na malalamiko yao kwenye Kliniki ya Ardhi inayoendelea katika siku yake ya tatu jijini hapa.

Senyamule alisema “nisisitize tunaposhughulikia kero hizi niombe wananchi wa Dodoma na kutoa wito najua kuna watu wanajirudiarudia kila wakati ambao kero zao zilishafungwa ila wanajaribu bahati nasibu nyingine. Nitoe rai wale ambao kero zao zilishafungwa huna haja ya kutumia masaa yako hapa, utapata jibu lilelile ambalo ulishalipata. Tukimaliza tatizo lako tunalifunga na tunapeana taarifa, nakala ipo kwa Mkurugenzi, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa na Kamishna msaidizi wa Ardhi”.

Akiongelea suala la utoaji hati miliki, mkuu wa mkoa alisema kuwa changamoto ya kuchelewesha hati inakwenda kukatuliwa. “Kupitia mkakati huu tunakwenda kumaliza tatizo la kuchelewesha utoaji wa hati. Kuna watu wanadai hati kwa miaka mitatu, miwili na mmoja nab ado hawajapata. Leo mnatangaziwa kwamba tatizo la kuchelewa kutoa hati limekwisha na sasa mtakuwa mnapata hati kwa wakati. Kwa sababu ya mrundikano mkubwa wa hati uliokuwepo, tumesema zoezi hili litaendelea kila mwezi, wiki moja tutakuwa tunatengeneza kliniki ya kutoa hati” alisema Senyamule.

Aidha, alisema kuwa wataendelea kusikiliza kero za wananchi. “Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inasikiliza kero, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inasikiliza kero na Mkurugenzi anasikiliza kero. Niwahakikishie tumejipanga kwenye utatuzi wa kero za Ardhi. Tutahakikisha Ardhi haiendelei kuwa masononeko kwa wananchi wa Dodoma. Mheshimiwa Rais anafanya mambo makubwa Dodoma tunatakiwa kuyafurahia kwa Pamoja, siyo kufikiria kero za Ardhi” alisema Senyamule.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kuongea na wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alisema kuwa kliniki hiyo itafanya kazi kwa siku tano mfululizo. Kazi hiyo ilianza juzi wananchi 1,014 walijitokeza na wananchi 514 walisikilizwa. “Kwa siku ya kwanza tuliweza kutoa hati 240 na Katibu Tawala Mkoa alikuja na kutoa hati kwa baadhi ya wananchi waliokuwepo. Wananchi waliobaki juzi tuliendelea nao jana, kulikuwa na wananchi karibu 900 na wananchi 515 kati yao walisikilizwa na hati 234 zilitolewa. Leo hati zilizoandaliwa hadi sasa zimefika 60. Nikujulishe pamoja na kutoa hati, wataalam wanasikiliza kero mbalimbali za wananchi na majibu yanatolewa na zile zinatohitaji kwenda uwandani tunaweka ahadi ya kwenda na kuzifanyia kazi” alisema Alhaj Shekimweri.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.