• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanufaika wa mkopo wasisitizwa kufanya marejesho kwa wakati

Imewekwa tarehe: May 19th, 2025

Na. Aisha Ibrahim, UHURU

Afisa Maendeleo ya Jamii, Kata ya Uhuru, Saada Zahaze, amewasisitiza wanufaika wa mkopo wa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kuzingatia miongozo na sheria za utoaji mkopo ikiwa ni kutumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa na kufanya marejesho kwa wakati uliopangiwa kupitia mfumo jumuishi.

Mfumo huo jumuishi unatekelezwa kwa mujibu wa sheria kwa kutoa mikopo ya asilimia 10 katika Jiji la Dodoma kwa uwiano wa 4-4-2 yaani wanawake asilimia nne, vijana asilimia nne na watu wenye ulemavu asilimia mbili. 

Akitoa ufafanuzi kuhusu mgawanyo wa mikopo hiyo alisema kuwa Kata ya Uhuru wamesajili vikundi 52, kati ya hivyo 18 ni vya wanawake, 17 ni vijana na 17 ni vya watu mchanganyiko ambapo katika vikundi hivyo, 18 tayari vimeshapata mkopo huo.

Aliongeza kuwa, mikopo iliyotolewa kuanzia mwaka 2021 ni shilingi milioni 423 taslimu. Wanawake walipata mkopo wa shilingi milioni 203 na vijana shilingi 220 ambapo marajesho mpaka sasa ni milioni 277.7.

Alisema kuwa licha ya kuwepo kwa muitikio mkubwa wa vikundi hivyo, kumekuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo baadhi ya wanufaika kutorejesha mikopo hiyo na kuhamia maeneo mengine bila kutoa taarifa. “Changamoto ni kwamba vikundi vingi vinavyojisajili katika Kata ya Uhuru ni vya wafanyabiashara na kuna wakati baadhi yao wanafunga biashara na kuondoka bila kutoa taarifa na baada ya hapo hatujui ni wapi pa kuwapatia” alisema Zahaze.

Ili kukabiriana na changamoto katika utoaji wa mikopo hiyo alisema kuwa kamati ya mikopo imejipanga kuhakikisha kila kikundi kinakuwa na wakazi wa kata hiyo wasiopungua wawili ili iwe rahisi kuwapata wanufaika.

Aidha, alieleza kuwa wanatumia njia mbalimbali ikiwemo mikutano ya wananchi katika kila mtaa na kuzunguka katika mikusanyiko ya watu wengi ili kuelimisha jamii kuhusiana na suala la mikopo kwa vikundi maalum. “Sisi tunatoa elimu inayohusu suala la mikopo kwa vikundi maalum kwa kupita kwenye mikutano ya wananchi inayofanyika ndani ya mitaa yetu. Pia tunazunguka kwenye maegesho ya bodaboda na vikundi vya mama lishe kutoa elimu” alieleza.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma atoa pongezi kwa Madiwani

    May 25, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.