• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watumishi wa Serikali Dodoma wamshukuru Rais Samia

Imewekwa tarehe: May 30th, 2022

Na. Moses Mpunga, DODOMA

WATUMISHI wa Serikali mkoani Dodoma wamemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha maslahi ya watumishi wa Umma kwa kupandisha mishahara kwa asilimia 23.3 pamoja na posho mbalimbali.

Shukrani hizo zilitolewa na Mtunza Kumbukumbu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Imelda Matofali katika hafla fupi ya kumshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuboresha maslahi ya watumishi katika ukumbi wa mikutano wa PSSSF jijini hapa.

Matofali akizungumza kwa niaba ya watunza kumbukumbu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, alimshukuru Rais kwa kuwakumbuka watumishi wa kada za chini. Alisema kuwa Rais amewakumbuka kwa kuwaongezea mishahara pamoja na posho jambo ambalo halikuwahi kufanyika kwa muda mrefu. "Kama mnavyojua Rais wetu ni mama na sifa kubwa ya mama ni kuwakumbuka watoto wake. Hivyo, tunamshukuru sana mama kwa kutukumbuka na sisi tunamuahidi kuchapa kazi kwa nguvu zetu zote" alisema Matofali.

Akiwawakilisha Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Afisa Mtendaji Kata ya Uhuru, Christina Mpete (pichani juu) alimuhakikishia Rais Samia Suluhu Hassan kuwa watumishi wataongeza juhudi katika kufanya kazi na kuwa atembee kifua mbele wao wapo nyuma yake na hawatamuangusha. Alisema kuwa ongezeko hilo la mishahara na posho limeongeza morali ndani ya watumishi wa Halmashauri hiyo.

"Mama yetu tunakuombea kwa Mwenyezi Mungu akulinde na akupe afya njema ili uendelee kuchapa kazi na kutuhudumia watanzania" aliongeza Mpete.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Mkoa wa Dodoma, Mwl. Samweli Malechela alisema licha ya kuongeza mishahara na posho, Rais amelipa malimbikizo mengi ya mishahara kwa watumishi ndani ya mwezi uliopita. Katika Mkoa wa Dodoma, walimu zaidi ya 2,300 walipandishwa madaraja.

Mwl. Malechela aliongeza kuwa kupanda kwa mishahara na posho kutaimarisha na kuboresha uchumi wa watumishi pamoja na watanzania kwa ujumla. Mzunguko wa fedha utakua ni mkubwa jambo litakalopelekea uchumi wa Taifa kukua pia, aliongeza.

"Licha ya mambo yote ya kuboresha maslahi ya watumishi anayoyafanya Mama Rais wetu mpendwa lakini bado miradi mikubwa inaendelea kwa kasi ileile. Kwahiyo, ni dhahiri kabisa kuwa mama anaupiga mwingi. Hivyo, ni jukumu letu kumuunga mkono kwa kufanya kazi kwa juhudi kubwa ili kuendena na kauli ya kazi iendelee" alimalizia Mwl. Malechela.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.