• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Jafo asifia hoteli mpya za Jiji, atarajia makubwa ya mfano

Imewekwa tarehe: December 30th, 2020

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo amesema anatamani kuona Halmashauri nchini zinajitegemea zenyewe kupitia mapato ya ndani katika kipindi cha miaka mitatu ijayo na kwamba ifike muda ziwe zinalipa watumishi wake mishahara.

Waziri Jafo alitoa kauli hiyo Disemba 29, 2020 wakati alipotembelea ujenzi wa mradi wa 'Government City Complex' unaojengwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika eneo la Mji wa Serikali Mtumba unaogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 59.3 hadi kukamilika kwake ambapo ametumia nafasi hiyo kulipongeza jiji la Dodoma kwa kutekeleza mradi huo kwa kutumia mapato yake ya ndani na siyo fedha za Serikali Kuu.

Alisema hakuna Halmshauri yoyote iliyofanya uwekezaji mkubwa nchini kama uliofanyika katika Jiji la Dodoma huku akieleza kuwa sasa analiona jiji hilo kupitia viongozi wake kuwa wapo kwenye sura hiyo anayoitamani.

“Hakuna halmashauri yoyote iliyofanya uwekezaji mkubwa kama huu hivyo nawapongeza Jiji la Dodoma, nataka jengo hili liwe kielelezo na kama nilivyosema mimi matamanio yangu nataka nione halmashauri zinazoweza kujitegeme zenyewe ifike muda halmashauri iseme hata nikiwa na watumishi wangu nitawalipa mimi mwenyewe natamani itokee ndani ya miaka mitatu ijayo,” alisema Waziri huyo wa TAMISEMI.

Ameendelea kufafanua kuwa, analiona Jiji la Dodoma lipo kwenye ndoto zake za kuona Halmashauri zikijitegemea, kupitia hoteli hiyo kubwa itakayokuwa na kumbi kadhaa kubwa za mikutano iliyojengwa katika Mji wa Serikali, pamoja na hoteli nyingine ya Dodoma City Hotel yenye ghorofa 11 iliyojengwa na Jiji hilo na inatarajiwa kuanza kutumika wakati wowote kuanzia sasa ikiwa katikati ya Jiji hilo eneo la Paradise.

“Nikiiangalia hoteli kubwa iliyopo mjini ya ghorofa 11 (Dodoma City Hotel), nikiangalia soko lenu la Dodoma (Job Ndugai Market), nikiangalia eneo la maegesho ya magari Nala (Nala Lory Park), eneo la mapumziko na michezo Chinangali (Chinangali Recreational Park) na Kituo Kikuu cha Mabasi Dodoma, ninapata uhakika kwamba Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaenda kujitegemea” alisisitiza Waziri Jafo.

Waziri ameutaka uongozi wa jiji la Dodoma kuhakikisha wanakwenda kusimamia kazi hiyo kwa kiwango cha juu ili iwe nzuri na ya mfano ambapo mtu akija ajifunze na kumtaka mkandarasi kutulia na kufanya kazi kwa uangalifu mkubwa, huku akimtaka kuongeza kasi ya ujenzi.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Mkurugenzi wa Jiji hilo Joseph Mafuru alisema mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 59.3 kwa awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza ni ujenzi wa jengo la 'Tower B' lenye ghorofa tano na kumbi tano za mikutano zenye uwezo wa kuchukua watu 1297.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.