• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: February 8th, 2025

Na. Aisha Ibrahim, DODOMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa (Mb), aliwapongeza watumishi wa umma kwa kusimamia miradi mbalimbali jijini Dodoma ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aliyasema hayo katika Hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Soko Kuu la Majengo pamoja ujenzi wa kituo cha daladala eneo la Mshikamano, Kizota na Nzuguni, iliyofanyika kiwanja cha Chinangali Park, Jijini Dodoma.

Akizungumzia kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali Mohamed Mchengerwa, alitaka wakandarasi wote ambao hawajatekeleza majukumu yao katika miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara, kutopewa  fursa ya kufanya kazi yoyote  ikiwa ni onyo kwa wale wote wanaofanya kazi kwa uzembe na kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa wakati.

"Maelekezo yangu kwa mtendaji mkuu na katibu mkuu wa TARURA, Mkandarasi huyu asiruhusiwe kufanya kazi yoyote chini ya TARURA kuanzia sasa mpaka akamilishe mradi huu tunaoukusudia, pamoja na wengine ambao hawajakamilisha miradi hii ambayo ilipaswa ikamilike mwezi Februari, wasiruhusiwe kufanya kazi yoyote hata ya shilingi 500" alisema Mchengerwa.

Sambamba na hayo, alisisitiza kuwepo kwa utaratibu mzuri wa kuingia na kutoka katika eneo la Stesheni ya reli Jijini Dodoma ili wananchi  na hata wageni kutoka nje ya Dodoma wajivunie uwepo wa Stesheni hiyo.

"Nawataka wakurugenzi wote wa majiji hasa Mkurungezi wa Jiji hili la Dodoma ambapo ni makao makuu ya nchi, mkuu wa Mkoa, Mkuu wa wilaya nendeni pale eneo la Stesheni ya reli na muweke utaratibu mzuri wa kuingia eneo hilo ili watanzania wanaokwenda na kurudi Jiji la Dodoma waweze kulifurahia jiji hili" alisema Mchengerwa.

Kwa upande wake Waziri wa madini, Anthony Mavunde (Mb) alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la

Dodoma ndiyo inayoongoza kwa mtandao mkubwa wa barabara zenye kiwango cha lami ambazo zina jumla ya urefu wa Kilomita 249.12 nchini Tanzania.

"Katika Halmashauri zote nchi nzima, Halmashauri ya Jiji la Dodoma ndiyo inaongoza kwa mtandao mrefu wa barabara za kiwango cha lami, sisi tuna Kilomita 249.12 ikifuatiwa na Halmashauri ya wilaya ya Kinondoni, wana urefu wa barabara wenye Kilomita 223" alisema Mavunde.

Aidha, aliendelea kwa kusema kuwa kumekuwa na kero mbalimbali katika vivuko vya maji katika maeneo ya Chaduru, Maili Mbili na Ntyuka ikiwemo wanafunzi kukwama na kushindwa kupita katika vivuko hivyo wakati wa mvua jambo linalopelekea  kutofika shuleni kwa wakati.

"Vivuko hivi imekuwa ni kilio kikubwa, mvua inaponyesha watoto wanaotoka upande wa pili wamekuwa wakishindwa kuvuka lile Korongo na wamekuwa wakishindwa kwenda shule" alisema Mavunde.

Nae, Mtendaji mkuu, Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA), Mhandisi Victor Seif, alisema lengo kuu la mradi wa "TACTIC" ni kuboresha usimamizi wa ukuaji wa miji pamoja na kuziwezesha Halmashauri za miji na majiji kutoa huduma bora kwa wananchi ikiwemo ujenzi wa miundombinu.

Alifafanua kuwa, kazi za ujenzi zinazofanyika katika mkataba wa "Package 1" ni Barabara ya Mbuyuni SP2 (Kilomita 1.69), Barabara ya Mauma-Makutano (Mita 760), Barabara ya Mbuyuni-Mwangaza (Kilomita 2.56), Barabara ya Ntyuka-Mkalama-Mapinduzi (Kilomita 5.2), Mtaro wa maji ya mvua Ilazo (Kilomita 2.1) na Uboreshaji wa mabwawa  ya kuhifadhia maji ya mvua (3) na mitaro ya kutiririsha maji (Kilomita 2.81).

Lakini, aliongeza kuwa kazi za ujenzi zinazotarajiwa kufanyika katika Mkataba wa "Package 2 ni Uboreshaji wa Soko Kuu la Majengo pamoja na kituo cha daladala eneo la Mshikamano, Uboreshaji wa Stendi ya mabasi madogo eneo la Kizota, Uboreshaji eneo la mabasi madogo eneo la Nzuguni na Ujenzi wa Vivuko maji katika maeneo ya Chaduru, Mailimbili na Ntyuka.

Katika eneo la mabasi madogo (daladala) kutakuwa na maeneo matatu yaliyopangiwa kwaajili ya daladala kuruhusu urahisi wa kuingia na kutoka yenye makinga mvua au jua, taa za kutumia umeme jua, choo cha kulipia na eneo litakaloweza kupangwa wafanyabiashara.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.