• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Mkuu, Rais wa CAF wakutana Jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: August 14th, 2021

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa jana amekutana kwa mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF), Bilionea Patrice Motsepe ofisini kwake Mlimwa hapa Jijini Dodoma na kujadiliana naye masuala muhimu ya kuendeleza michezo nchini.

Motsepe, raia wa Afrika Kusini na mmiliki wa klabu ya Mamelod Sundows yupo nchini kwa mwaliko wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia na leo anatarajiwa kuhudhuria fainali ya Kombe la Kagame kati ya Expresa ya Uganda na Nyasa Big Bullets ya Malawi mchezo utakaochezwa katika dimba la Benjamin Mkapa kuanzia saa 1 kamili usiku Jijini Dar es Salaam. 

Waziri Mkuu alimweleza mikakati ambayo Serikali inatumia ili kuinua kiwango cha soka nchini. "Sisi tumeanza kuboresha michezo nchini chini ya mpango unaohusisha Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mpango huu unalenga kuibua vipaji vya vijana kupitia mashindano ua UMITASHUMTA, UMISETA, Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati." Alisema.

Katika mazungumzo yao, walijadiliana suala la kuendelea kutenga bajeti ya kuinua michezo kwa vile nchi nyingi zinashindwa kufanya vizuri kwenye michezo kwa sababu hazitengi bajeti. "Nimemweleza kuwa hapa kwetu kupitia Bunge letu tukufu, tumekuwa tukitenga bajeti hiyo japokuwa tunajua kuwa haitoshelezi mahitaji yote.

Kuhusu uendelezaji wa michezo nchini, Rais wa CAF ametusihi tuwe na mpango madhubuti wa kupata maeneo ya kufanyia mazoezi, tuwe na viwanja bora vyenye vipimo vya kisasa, jambo ambalo nimemweleza linatekelezwa na shirikisho la soka nchini. Pili, ametutaka tuandae vijana kuanzia umri mdogo, tuwe na taasisi za Serikali na za sekta binafsi zinazofundisha soka, waamuzi na makocha ili tuwaibue akina Samatta wengi zaidi kwani na sisi tunaamini kuwa wapo."

Naye Dkt. Motsepe amesema katika uongozi wake amelenga mambo makuu matatu ambayo ni sekta binafsi kuwekeza kwenye michezo na kuongeza udhamini, ujenzi wa vituo vya michezo na vituo vya kuendeleza vijana.

Amesema chini ya mfuko wa dola bilioni mona amedhamiria kuimarisha miundombinu ya michezo. Kuna baadhi ya nchi za Afrika zina viwanja vikubwa vya micjezo lakini havijakidhi vigezo vya FIFA. Tunataka na wao wafikie viwango vya kimataifa.

Motsepe amesifu kuwa timu ya Taifa ya Tanzania ina uwezo kuwa timu bingwa barani Afrika kutokana na umahiri walionao hivi sasa na ametumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuunga mkono michezo nchini ambapo wiki ijayo atapokea kombe la CECAFA - 2021 la vijana wenye umri chini ya miaka 23.

Kiongozi huyo wa shirikisho la mpira Afrika ameipongeza Tanzania kwa kuwa nchi ya kuigwa kutokana na wananchi wake wengi kupenda michezo na hasa kunapokuwa na mechi zinazokutanisha vilabu vikubwa nchini kwa vile zinawaleta mashabiki hata kutoka nchi jirani.

Ikumbukwe Jiji la Dodoma linamiliki timu ya Dodoma Jiji FC inayoshiriki katika ligi kuu hapa nchini Tanzania. 


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.