• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

'Vita' dhidi ya Malaria, Waziri Ummy apongeza Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: April 24th, 2019

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa jitihada kubwa zilizofanyika kwa ajili ya kutokomeza ugonjwa wa Malaria.

Waziri Ummy ametoa pongezi hizo leo wakati alipokuwa anagawa vyandarua vyenye dawa kwa akinamama wajawazito na wenye watoto wadogo katika kituo cha Afya cha Makole Jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetokomeza ugonjwa wa Malaria kutoka asilimia 1 mpaka asilimia 0.6 ikiwa ni mafanikio makubwa, ambapo amesema katika kipindi cha miaka mitatu nchi nzima ugonjwa wa Malaria umeweza kupungua kutoka asilimia 14 mwaka 2015 mpaka asilimia 7 mwaka 2018.

"Toka Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Mhe. John Magufuli iingie madarakani tumeweza kutekeleza mikakati mbalimbali ya kutokomeza Malaria nchini, katika kipindi kifupi cha miaka mitatu tumeweza kupunguza Malaria zaidi ya asilimia 50 kutoka asilimia 14 mwaka 2015 mpaka asilimia 7 mwaka 2018", alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy aliwasifu akinababa walioleta watoto wao kliniki katika kituo hicho na  amewataka wananchi kwa ujumla kutimiza wajibu wao ili kutokomeza Malaria kama kauli mbiu ya mwaka huu inavyosema "Ziro Malaria inaanza na mimi", hivyo amewataka wakina mama wajawazito kuhudhuria kliniki kwa ajili ya uchunguzi wa afya zao na kufanyiwa vipimo vyote kikiwemo cha Malaria.

Waziri huyo alibainisha kuwa, Tanzania bado haijafanya vizuri katika takwimu za akina mama wajawazito kuhudhuria kliniki ambapo katika akinamama wajawazito 100 ni akinamama 29 ndiyo wanaohudhuria kliniki mara nne katika kipindi cha ujauzito.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mratibu wa Malaria wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Francis Bujiku alisema mafanikio ya kutokomeza Malaria katika jiji la Dodoma yamekuja baada ya utekelezaji wa afua mbalimbali za Malaria ikiwa ni pamoja na kuhakikisha tiba sahihi za Malaria zinazotolewa katika vituo vyote vya afya, elimu ya kujikinga na ugonjwa huo, pamoja na Mkoa kufanikiwa kuangamiza viluilui wa mbu kwa kunyunyizia dawa kwenye mazalia yao.

Bujiku alisema mwaka 2015 Mkoa uliendesha zoezi la ugawaji vyandarua vyenye dawa kwenye ngazi ya kaya, ambapo takribani vyandarua milioni moja na laki tano viligawiwa kwa wananchi, huku akina mama wajawazito waliofika kliniki kwenye hudhurio la kwanza la ujauzito na watoto chini ya mwaka mmoja waliofika kupata chanjo ya surua nao wakipewa vyandarua hivyo.

Waziri Ummy Mwalimu akimuangalia mtoto aliyeletwa kliniki ya Kituo cha Afya Makole kilichopo Jijini Dodoma 

kwa ajili ya kupata chanjo wakati alipotembelea kituo hicho na kugawa vyandarua vyenye dawa kwa 

wanawake wajawazito na watoto walio na umri chini ya mwaka mmoja.

Waziri Ummy Mwalimu akimpongeza baba aliyeleta mtoto kliniki kwa ajili ya kupata chanjo katika kituo cha 

Afya Makole Jijini Dodoma.

Waziri Ummy Mwalimu akiwa na baadhi ya akinamama waliopewa vyandarua baada ya kufika kliniki katika 

kituo cha Afya cha Makole Jijini Dodoma wakati Waziri alipofika na kugawa vyandarua hivyo.




Chanzo: afyablog.moh.go.tz (afyablog.moh.go.tz)

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.