• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wenyeviti wa mitaa Dodoma wahimizwa kutoa huduma bora

Imewekwa tarehe: March 5th, 2025

Na. Halima Majidi, MTUMBA

Wenyeviti wa mitaa jijini Dodoma wametakiwa kutambua na kusimamia majukumu yao ipasavyo kwa kuwapatia huduma bora na kuwashirikisha wananchi katika miradi mbalimbali ili kuleta tija katika ulinzi na utunzaji wa miradi hiyo.

Hayo yalisema na Mwezeshaji wa Mafunzo ya Uongozi na Utawala bora, Mwinyipembe Victor, wakati akitoa mafunzo hayo kwa wenyeviti wa mitaa yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba.

Victor alisema kuwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ndogo ya 146 dhumuni la kuwepo kwa serikali za mitaa nikupeleka madaraka kwa wananchi, hivyo wenyeviti wa mitaa wanatakiwa kukumbuka na kutekeleza madaraka yao. “Wenyeviti wa mitaa tumekuwa tunajisahau sisi tunakuwa mabosi halafu wananchi wanakuwa wanahangaika, mwananchi atahangaika ndani ya miaka mitano ambayo umemnyanyasa ila ipo siku na wewe utahangaika” alisema Victor.

Aidha, aliwasitiza wenyeviti wa mitaa kutowaacha nyuma wananchi badala yake kuwachukulia kama wao ndio waajiri wao kwa kutekeleza dhamana zao ikiwemo kuwatumikia na kuwahudumia ipasavyo. “Lengo la kuwashirikisha wananchi katika miradi ya maendeleo ni  kutengeneza ari ya umiliki, mwananchi akishirikishwa katika kupanga hata kwenye kulinda na kutunza lazima atatekeleza tu, serikali ya mtaa itafanya vizuri endapo  mwananchi atapewa madaraka yake” alisisitiza Victor.

Sanjari na hayo aliongeza kuwa moja ya majukumu ya serikali ya mtaa ni kuhakikisha utekelezaji wa sheria za ulinzi wa wananchi pamoja na kuwepo kwa demokrasia katika mitaa. Pia kazi ya serikali ya mtaa ni kuhakikisha wanasimamia taratibu zote zinazohusu mpango mji.

“Kuna sheria inayohusu urembeshaji miji hatuwaambii tu wananchi kuwa wapake rangi ili mtaa upendeze hapana ni sheria inatutaka tuwe na utaratibu wa kuhakikisha mitaa yetu inapendeza na kwa hapa Dodoma tumeanzisha utaratibu wa kuezeka bati la rangi fulani ni kwaajili ya mtaa fulani. Haya yote ni majukumu ya serikali za mitaa” aliongeza Victor.

Nae, Mwenyekiti wa Mtaa wa Sogeambele, Kata ya Chihanga, Meshack Joseph, alisema kuwa anashukuru kwa mafunzo kwasababu yamemfundisha kuwa na weledi katika shughuli anazotakiwa kuzifanya. Pia yamemjengea uwezo wa kujiamini katika utendaji wa kazi. “Kwasababu sehemu nyingine tulikuwa tunafanya kwa kupapasa papasa kwa kujua kwamba nikifanya hiki nitakuwa nimekosea lakini kumbe baadhi ya mambo tulikuwa tunaenda sawa lakini tulikuwa tunaenda kwa kutojiamini. Hivyo, mafunzo haya yametujengea uwezo wa kujitambua, kama mwenyekiti majukumu yangu ni yapi” alisema Joseph.

Alifafanua kuwa katika mafunzo hayo alijifunza sehemu kubwa kuhusu namna ya kuwashirikisha wananchi wake katika masuala mbalimbali yanayohusu mtaa wake ikiwemo utoaji wa maamuzi. “Katika utekelezaji wa mambo yangu, cha kwanza kabisa nikufanya taratibu za kuwashirikisha wananchi wangu katika maamuzi ya mambo yote ninayotaka kwenda kuyafanya kwenye mtaa wangu na pia nitaangali taratibu nyingine za kuibua miradi mbalimbali kwa manufaa ya wananchi wangu” alifafanua Joseph.

Upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Nyumba 300 Nzuguni, Donata Zitatu alisema kuwa, amefurahi sana kwa mafunzo hayo, kwasababu yamemuwezesha kujua mipaka yake na utendaji kazi kama mwenyekiti pamoja na kusimamia mtaa wake, pia amejifunza namna ya kuanzisha vyanzo vya ndani vya mapato pamoja na kubuni miradi ya ndani itakayowasaidia kuingiza mapato ya ndani. “Mambo mengi tulikuwa tunaenda tu lakini semina ya leo imenisaidia na imenigusa sana, natoa shukrani zangu kwa wadau, Mkuu wa Wilaya, Shekimweri pamoja na Mkurugenzi wa Jiji kwa kubuni semina hii kwaajili yetu, kwasababu imetufundisha mambo mengi kama wenyeviti” alisema Zitatu.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.