• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

WILAYA YA DODOMA YAWAPATIA ZAWADI KINA MAMA WALIOJIFUNGUA KATIKA KITUO CHA AFYA MAKOLE

Imewekwa tarehe: December 7th, 2023

Na. Dennis Gondwe, MAKOLE

MIAKA 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara Wilaya ya Dodoma imewapatia zawadi kina mama waliojifungua katika Kituo cha Afya Makole na kuwatakia heri na kuwahakikishia kuwa serikali inataendelea kutoa huduma bora kwao.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipoongoza timu ya wataalam wa wilaya na halmashauri kukagua hali ya huduma katika Kituo cha Afya Makole, kutembelea kina mama wanaotarajia kujifungua na waliojifungua na kuwapatia zawadi mbalimbali.

Alhaj Shekimweri alisema kuwa Wilaya ya Dodoma katika kuelekea maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara imetembelea Kituo cha Afya Makole kukagua hali ya utoaji huduma. “Kwa niaba ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan tumekuja kuona huduma zinatolewaje hapa sehemu ya kujifungulia.  Tunafahamu hapa kuna wastani wa kujifungua kawaida wanawake kati ya 15-25 kwa siku na wale wanaojifungua kwa upasuaji ni kati ya 4-6 kwa siku. Hii ni idadi kubwa hivyo, tuna hamu ya kupata mrejesho wa huduma hizo. Lakini pia kuwaletea zawadi ndogo ya kuadhimisha miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania bara tukiamini kuwa uhuru huu siyo tu wa kujitawala lakini wa kujiletea maendeleo. Kina mama wajawazito kupata huduma nzuri za kliniki wakielekea kujifungua, wajifungue katika maeneo salama katika vituo vya kutolea huduma kama hapa Kituo cha Afya Makole. Na haya ndiyo matunda ya uhuru wetu” alisema Alhaj Shekimweri.

Alisema kuwa Rais, amefanya mambo makubwa katika sekta ya Afya. “Mheshimiwa Rais, anatujengea hospitali ya wilaya, tayari ametuletea shilingi 1,500,000,000 za kujenga hospitali hiyo na hapa Makole ametuletea shilingi 750 za kuboresha huduma za Afya. Tumekuja kuwasalimia na tunaendelea kuwaombea heri kwa Mungu na tunawapenda na tunawathamini na tupo hapa kuonesha upendo huo” alisema Alhaj Shekimweri.

Akitoa taarifa fupi ya huduma kwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alisema kuwa watu wengi wanapenda kujifungua katika Kituo cha Afya Makole kutoka na ubora wa huduma. “Tumekuwa tukipata kina mama takribani 20 wanaojifungua kila siku katika kituo hiki. Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kama ulivyoona kuna kimama takribani 47 waliolazwa na waliojifungua katika kituo hiki. Tunashukuru tunapopata matokeo kuwa wanajifungua salama ndiyo dhamira ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuona kina mama wanajifungua salama lakini na watoto wao wakiwa salama” alisema Dkt. Method.

Kwa upande wa mama aliyejifungua katika kituo hicho, Stella Gilbert alisema huduma ni nzuri. “Nimejifungua leo saa sita mchana katika Kituo cha Afya Makole tena nimejifungua salama mtoto wa kiume. Nawashukuru madaktari na wauguzi wanahudumia vizuri na wanajali sana wagonjwa, Mungu awabariki sana. Hali ya huduma ni nzuri sana” alisema Gilbert.

Katika kuelekea miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara, Wilaya ya Dodoma ilitembelea Kituo cha Afya Makole kukagua hali ya utoaji huduma katika wodi ya kima mama, kuwatia moyo kina mama wanaotarajia kujifungua na waliojifungua na kuwapatia zawadi mbalimbali.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.