• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Fedha kushirikiana kuelimisha jamii

Imewekwa tarehe: June 30th, 2023

Na WMJJWM, DODOMA

WIZARA ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum inajipanga kutoa elimu ya masuala ya fedha kwa jamii hasa makundi maalum kwa kushirikiana na Wizara ya fedha na Mipango.

Hayo yamebainika kwenye mafunzo yaliyotolewa na Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango kwa Menejimenti na watumishi wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, kuhusu fursa zinazopatikana katika masuala ya fedha, leo Juni 30, 2023 jijini Dodoma.

Akifungua Mafunzo hayo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt Dorothy Gwajima, amesema ushahidi unaonesha kuwa, yapo makundi mengi ndani ya Jamii ambayo yanatamani kuchangamkia fursa za kiuchumi lakini wanashindwa kutokana na kutokuwa na taarifa ya wapi pakuanzia. Amesema Wizara itashirikiana kwa karibu zaidi na Wizara ya Fedha na Mipango kutoa elimu ya fedha kwa wataalamu ili wakaielimishe jamii hadi ngazi ya chini.

"Mwaka 2022 nilipata Bahati ya kutembelea Maonesho ya Saba Saba na kupita kwenye taasisi kadhaa za fedha ambapo nilibaini uwepo wa fursa ambazo wanajamii wengi hawazifahamu" amesema Waziri Dkt. Gwajima.

Aidha Waziri Dkt. Gwajima amesema mafunzo hayo yanasaidia kubadili fikra kuanzia ngazi ya watendaji ili wawe daraja imara kuwafikia wananchi kwa taarifa sahihi hasa wanawake na makundi maalum ndani ya jamii.

Kwa upande wake Kamishna wa sekta ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Charles Mwamwaja amesema Jamii ina kila sababu ya kuelimishwa kuhusu fursa na matumizi ya fedha katika maisha yao ya kila siku na kubadili utaratibu wa nidhamu ya fedha kwa kuwa na utaratibu wa kuweka akiba.

Dkt. Mwamwaja amebainisha kuwa, tafiti nyingi zilizofanyika zinaonesha watu wengi hawana uelewa mpana wa fursa zilizopo katika Sekta ya fedha, hivyo kupitia Wizara fedha wameendelea kutoa Elimu hiyo kwenye Jamii.

"Uwekaji wa akiba ni suala la msingi sana, unapoona miradi mikubwa inafanyika leo hii, ni kwa kuwa tunajua tukishaweka miundombinu hii inachangia sana ukuaji wa uchumi, barabara, maji, umeme nk. vinapofika lazima thamani ya eneo hilo inakuwa juu zaidi." Amesema Dkt. Mwamwaja.

Naye Mtaalam wa fedha Bi. Dionisia Mjema, anayesimamia huduma ndogondogo za Kifedha kutoka Wizara ya Fedha, ameelezea mkakati wa Programu ya Elimu ya fedha kwa Umma pamoja na kusisitiza suala la uwekezaji kwenye Masoko ya hisa.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt Dorothy Gwajima katika picha ya pamoja na wahitimu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.