• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

2022/2023 Wilaya ya Dodoma ilizalisha tani 48 za mazao ya chakula na biashara

Imewekwa tarehe: October 4th, 2023

 Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WILAYA ya Dodoma ilizalisha tani 48,413 za mazao ya chakula na biashara katika msimu wa kilimo wa mwaka 2022/2023 ukiifanya hali ya chakula kuwa ya wastani.

Taarifa hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma risala ya utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Chamwino jijini Dodoma.

Mbugi alisema “Mheshimiwa Rais; hali ya chakula kwa sasa ni ya wastani kutokana na mavuno yaliyopatikana msimu wa kilimo wa mwaka 2022/2023. Wilaya ilizalisha tani 48,413 za mazao ya chakula na biashara. Katika msimu wa kilimo wa 2022/2023 eneo lililolimwa kwa ajili ya mazao ya chakula ni hekta 18,522 ambazo zilizalisha tani 23,682 za mavuno. Kwa mazao ya biashara eneo lililolimwa ni hekta 20,869 na zilizalisha tani 24,731. Bei za vyakula sokoni ni za wastani. Shilingi 18,653,976 zimetumika kutekeleza miradi ya ukarabati wa Bwawa la Umwagiliaji Ipala na shamba la mafunzo la Msalato”.

Akiongelea sekta ya mifugo alisema kuwa wilaya ilitoa shilingi 26,927,000 kwa ajili ya zoezi la chanjo ya homa ya mapafu kwa ng’ombe na mbuzi. “Ng’ombe 41,258 na mbuzi 9,370 walichanjwa. Shilingi 9,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa “shade“ za mizani mbili ya ng’ombe zilizotolewa na serikali katika mnada wa Hombolo na Msalato. Serikali ilitoa ruzuku ya dawa lita 96  za kuogeshea mifugo, shilingi 5,008,000 kwa ajili ya ujenzi wa birika la kunyweshea mifugo katika Kata ya Ipala. Wilaya ilitoa shilingi 16,670,650.00 kwa ajili ya ujenzi wa makaro mawili na shilingi 15,800,000 kwa ajili ujenzi wa uzio wa mifugo“ alisema Mbugi.

Kuhusu sekta ya uvuvi alisema kuwa wananchi walihamasishwa kuanzisha mabwawa 123 ya samaki kwa ajili ya kuboresha kipato na lishe. “Shirika la Save the Children lilitoa msaada wa vifaranga vya samaki aina ya Sato kwa wafugaji wanne na kikundi kimoja katika Kata za Msalato, Miyuji, na Hombolo Makulu. Vifaranga 6,000 vilipandwa na chakula cha Kg 150 kilitolewa” alisema Mbugi.

Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 unaongozwa na kaulimbiu isemayo “Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya Maji kwa ustawi wa Viumbe Hai kwa Uchumi wa Taifa”

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.