• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

CCTV kamera mwarobaini wa wavunjifu wa sheria jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: October 2nd, 2025

Na. Hellen M. Minja

Habari – DODOMA RS

Wito umetolewa kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma kubadilika kwa kufuata Sheria za nchi kwani pasi na hivyo, watafichuliwa kupitia Mfumo wa kisasa wa Kamera za barabarani na mitaani (CCTV) zilizofungwa kwenye maeneo kadhaa ya Jiji la Dodoma wakifanya matendo ya kihalifu na watachukuliwa hatua za kisheria.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameyasema hayo Septemba 30, 2025 alipokua kwenye ziara ya ukaguzi wa Mradi wa kusimika Kamera za barabarani kwenye maungio ya barabara za kuingia na kutoka Mkoa wa Dodoma kwa lengo la kuimarisha ulinzi ndani ya Jijini hili la Makao Makuu ya nchi.

“Nitoe wito kwa wananchi wa Dodoma wabadilike kwa kufuata sheria na taratibu za nchi kwani wasipofanya hivyo wataonekana kupitia Mfumo wa Kamera za barabarani wakifanya uhalifu na watakapoonekana wakitenda kinyume cha taratibu, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao”.

Aidha, Mhe. Senyamule ameongeza kuwa kupitia Teknolojia hiyo ambayo Kamera zitawekwa kwenye maeneo makubwa, italeta sifa kwa wageni kuingia na kuwekeza kutokana na uhakika wa usalama hivyo amewaasa wananchi kuilinda miundombinu ya Serikali kwani imewekwa kwa faida yao.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri amesema zoezi hilo lililogharimu kiasi cha shilingi Milioni 473, linaunga mkono juhudi za ujio wa Serikali Mkoa wa Dodoma pamoja na kutimiza ndoto ya Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuifanya Dodoma kuwa sehemu salama kwa uwekezaji na utalii.

Vile vile, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Wislance Smart System Bw. Wisley A. Ussiri ambao wanatekeleza Mradi huo amesema Mradi huo umelenga njia kuu nne za kuingia na kutoka Jiji la Dodoma ambapo utekelezaji wake umefikia 90% na Kamera zilizofungwa ni za kisasa zenye kuleta tija kwani zinaonesha picha zenye ubora wa hali ya juu.

Mradi wa kusimika Kamera za barabarani katika Mkoa wa Dodoma umetumia siku 90 sawa na Miezi mitatu ya utekelezaji ambapo nguzo 50 zilizobeba jumla ya Kamera 106 zenye uwezo wa kutumia teknolojia ya kisasa ya Akili Mnemba zimesimikwa.

Matangazo

  • Tangazo na Orodha ya Walioitwa kwenye mafunzo ya Wasimamizi, Wasimamizi wasaidizi na Makarani Jimbo la Dodoma Mjini na Mtumba October 23, 2025
  • TANGAZO LA MABADILIKO YA TAREHE YA USAHILI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA WASIMAMIZI JIMBO LA MTUMBA October 03, 2025
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA- DODOMA MJINI October 03, 2025
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Rc Senyamule awasihi wawekezaji sekta binafsi kuwekeza Dodoma

    October 03, 2025
  • CCTV kamera mwarobaini wa wavunjifu wa sheria jiji la Dodoma

    October 02, 2025
  • Wadau wa afya wapongezwa kwa juhudi zakudhibiti vifo vya wajawazito

    October 01, 2025
  • UONGOZI WA KLABU YA MICHEZO OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WAKUTANA NA RAS KAZUNGU

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.