• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Afisa Elimu Jiji la Dodoma aagiza midahalo kufanyika ngazi ya Shule

Imewekwa tarehe: October 13th, 2022

Na. Theresia Nkwanga, Dodoma

AFISA Elimu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Upendo Rweyemamu amesema mashindano ya Mdahalo kwa shule za Sekondari yafanyike kwenye ngazi ya shule ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kujiamini , kuzungumza , kujielezea na kuandika kwa lugha ya Kiingereza.

Hayo aliyasema alipohudhuria fainali za Mashindano ya Mdahalo kwa shule za Sekondari Dodoma yaliyofanyika tarehe 10 Oktoba,2022  katika ukumbi wa Dodoma Sekondari.

Rweyemamu alisema kumekuwa na mashindano ya mdahalo kwa shule za Halmashauri ya Jiji la Dodoma ngazi ya Wilaya ni wakati sasa mashindano yafanyike kwenye ngazi ya shule kati ya darasa na darasa ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kuzungumza na kuandika kwa lugha ya Kiingereza.

Akiongelea umuhimu wa midahalo katika taaluma Rweyemamu alisema midahalo inamjengea mwanafunzi ujasiri wa kujielezea , kujenga hoja, inamuongezea misamiati ya lugha ya kiingereza, inamjengea ujasiri pia inaongeza ufaulu kwa wanafunzi.

“Tunaenda kuongeza ufaulu katika shule zetu sababu wanafunzi wanaenda kuwa vizuri kwenye lugha ya kiingereza, mwanafunzi anaweza akawa ameelewa swali lakini hana misamiati yakutosha ataishia kujua kichwani mwake lakini atashindwa kuweka kwenye maandishi kupitia midahalo mwanafunzi ataongeza misamiati na kumudu masomo yake pamoja na mitihani anayoulizwa kwa lugha ya kiingereza”, alisema Rweyemamu

Kwa upande mwingine, Mratibu wa shindano la Mdahalo kwa shule za Sekondari Dodoma, Malick Masoud alisema lengo la mashindano haya nikuwajengea wanafunzi uwezo wa kujiamini, kuwakuza kitaaluma, kuchangamsha ubongo wao kupitia mada mbalimbali zinazojadiliwa  pia kuwakutanisha pamoja kama wanafunzi wa Dodoma .

Aliongezea kwa kuzipongeza shule zote zilizoshiriki mashindano ya Mdahalo kwa shule za Sekondari Dodoma na kuzitia moyo shule ambazo zilitoka mapema kwenye mashindano kutokukata tamaa pia alitoa chachu kwa shule ambazo hazijashiriki kujiandaa kwa awamu ijayo ya mashindano.

“Tumepokea simu nyingi kutoka kwa baadhi ya shule wakiuliza kwa nini sisi hatujashiriki, napenda kuwaambia huu ni mwanzo  tu awamu inayofuata shule zote za Halmashauri ya Jiji la Dodoma zitashiriki”.

Naye Nadhifa Ayubu, mwanafunzi kutoka Viwandani Sekondari alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri kwa kuanzisha shindano hili kwani linawajengea uwezo wa kujieleza mbele za watu hivyo, kuwafanya wajiamini pia kuelewa lugha ya kiingereza ambayo inatumika kujifunzia kwa elimu ya Sekondari.

Mashindano ya Mdahalo kwa shule za Sekondari Dodoma yalianza tarehe 01 Oktoba, 2022  yakihusisha  shule ya Mkonze, Mnadani, Miyuji ,Kisasa, Dodoma Sekondari, Viwandani, Sechelela, Nzughuni, Kikuyu, Hazina, Nghong’onha na Kiwanja cha Ndege na yalihitimishwa tarehe 10 Oktoba, 2022 huku shule ya Sekondari Miyuji ikiibuka mshindi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.