• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Afisa Elimu Sekondari Jiji la Dodoma awataka wanafunzi kufuatilia masomo yafundishwayo kwa njia ya redio

Imewekwa tarehe: May 7th, 2020

WANAFUNZI wote wa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufuatilia vipindi vinavyoendelea katika redio zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ili waweze kuendelea na program ya masomo wawapo nyumbani.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu alipokuwa akiongea katika kipindi cha ‘Dodoma Live’ kinachorushwa na kituo cha redio cha Dodoma FM jana asubuhi.

Mwalimu Rweyemamu amesema kuwa program ya kuwafundisha wanafunzi kupitia redio inalenga kuwafundisha wanafunzi walio katika madarasa ya mitihani. Madarasa hayo ni darasa la nne na darasa la saba kwa shule za msingi na wanafunzi wa kidato cha pili na nne kwa sekondari, amesema. Utaratibu huu ni mwanzo wa program hii, “mpango wetu ni kufundisha madarasa yote katika kipindi kijacho. Masomo haya tunayofundisha wanafunzi wote wanatakiwa kuyafuatilia. Mfano, tunapofundisha kidato cha pili, wanafunzi wa kidato cha tatu na cha nne wanaweza kufuatilia na kujifunza kama marejeo ya kile walichojifunza. Wanafunzi wa shule ya msingi vivyo hivyo” amesema Mwalimu Rweyemamu.

Akiongelea ratiba ya vipindi vya redio, amesema kuwa ratiba hiyo imeandaliwa kwa vipindi na redio zote katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Ratiba inapatikana katika tovuti ya Jiji, www.dodomacc.go.tz pamoja na “home packages zipo kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi kufanya mazoezi zaidi”. Ratiba hiyo pia inapatikana kwa walimu wakuu, wakuu wa shule na kwa maafisa elimu kata wote wa jiji la Dodoma. Aidha, tumewaandikia barua viongozi wa dini na kuwatumia nakala za ratiba hiyo ili wasaidie kuwafikishia waumini wao” amesema Mwalimu Rweyemamu.

Ikumbukwe kuwa mkakati wa kuwanusuru wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wa Jiji la Dodoma ulizinduliwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi tarehe 28 Aprili, 2020 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Afisa Elimu ya Msingi wa Jiji la Dodoma Mwalimu Joseph Mabeyo (kushoto) na Afisa Elimu ya Sekondari Mwalimu Upendo Rweyemamu (katikati) walipokuwa wakishiriki kipindi cha mahojiano cha 'Dodoma Live' katika redio ya Dodoma FM jana na kuelezea juu ya utekelezaji wa mkakati kufundisha wanafunzi walio nyumbani wakati wa kipindi hiki ambacho shule zimefungwa ili kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona. Kulia ni mtangazaji wa redio ya Dodoma FM.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.