• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Afya ya kinywa na meno kupatiwa mwarobaini - Prof. Rugaje

Imewekwa tarehe: November 21st, 2022

SERIKALI imesema itaendelea kuwekeza kwenye maeneo tofauti yanayohusu afya ya kinywa na meno na tasnia zinazoambatana na kada hiyo ili kuboresha afya ya Kinywa na Meno nchini.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa leo tarehe 21 Novemba, 2022 Jijini Mwanza katika Ukumbi wa TFDA na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Wizara ya Afya Prof. Paschal Rugaje wakati akifungua kikao kazi cha Waganga Wakuu wa Mikoa wa Afya ya Kinywa na Meno na baadhi ya Wataalam hao kutoka kwenye baadhi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Akimwakilisha Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumani Nagu, Prof. Paschal Rugaje amesema takwimu zinaonyesha kuwa watanzania wengi wanakabiliwa na matatizo makubwa yanayotokana na afya ya kinywa na meno kote nchini na ndiyo maana imeamua kuwekeza katika eneo hilo.

“Serikali imeendelea kuwekeza katika nafasi za mafunzo ya madaktari wa magonjwa ya afya ya kinywa na meno, pia tasnia nyingine ambazo zinaambatana na madaktari wasaidizi, wauguzi, mafundi wa mitambo kwa ajili ya meno (Biomedical Engineers), vifaa tiba vya meno na pia katika kuajiri watumishi” amesema Prof. Rugaje.

Aidha, amesema afya ya kinywa na meno ni muhimu sana na ni tatizo, kwani takwimu zinaonyesha kuwa katika kila watu wazima wanne, watatu wameoza meno, katika kila watoto watatu, mmoja ameoza meno na katika kila watu kumi mmoja anatatizo la fizi.  

Prof. Rugaje pia amesema kuwa kwa hali ilivyo sasa ni hospitali za Mikoa na za juu yake ndizo zinazotoa huduma ya afya na kinywa kwa uhakika lakini matarajio na mipango ya Serikali ni kuhakikisha kuwa vituo vya afya na hospitali za Halmashauri ziwe zinatoa huduma hiyo ifikapo mwaka 2025.

Kwa upande wake Dkt. James Kengia akiongea kwa niaba ya mkurugenzi wa Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema kwa hivi sasa Hospitali 142 za Halmashauri zinatoa huduma ya afya ya kinywa na meno.

Naye Dkt. Baraka Nzobo Kaimu Mkurugenzi anayeshughulikia huduma ya Afya ya Kinywa na Meno Wizara ya Afya amesema Wizara ya Afya itaendelea kutoa elimu kwa jamii kupitia vyombo mbalimbali vya habari pamoja na msisitizo wa elimu mashuleni ili kupata jamii yenye afya ya kinywa na meno.

Akitoa shukrani kwa niaba ya wajumbe, Dkt. Mohamed Mpunjo Mganga Mkuu wa Kinywa na Meno Mkoa wa Lindi amesema maelekezo yote ya Serikali yaliyotolewa ikiwa ni pamoja na machapisho, huduma, kubuni na kuandika maandiko ya miradi watayatekeleza kwa wakati.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.