• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ahadi ya Rais yaanza kutekelezwa Mpwapwa

Imewekwa tarehe: September 9th, 2020

AHADI ya Rais John Magufuli ya kuifungua Wilaya ya Mpwapwa kwa miundombinu imetimia katika muda mfupi kwa kuanza ujenzi wa barabara za lami na hivyo wilaya hiyo itaunganishwa na barabara kuu za Dodoma-Iringa na Dodoma-Morogoro hivi karibuni.

Rais Magufuli alitembelea wilaya hiyo mwaka jana na kuahidi kutoa fedha kujenga miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami Mpwapwa ambayo ni wilaya kongwe lakini ina kipande cha kilometa moja tu ya barabara ya lami mjini hapo.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Jabir Shekimweri akizungumza wakati wa ziara ya siku mbili ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyopewa fedha na serikali, alisema ahadi ya Rais imeanza kutekelezwa katika muda mfupi na wilaya hiyo imekuwa na barabara za lami.

Shekimweri alimpongeza Rais John Magufuli kwa ahadi aliyotoa ya kujenga barabara za lami kilometa tano mjini hapo, ambapo tayari Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) imeshajenga kilometa tatu kati ya tano.

Shekimweri alisema pia barabara ya Mpwapwa - Kongwa itajengwa kilometa 30 kutokana na ahadi iliyopo ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya 2020-2025, hivyo barabara hiyo itajengwa kilometa 35 na itabakia kidogo kuunganishwa na lami wilayani Kongwa.

Pia wilaya hiyo itafunguka kwa barabara ya lami kutoka Mpwapwa-Kibakwe yenye urefu wa kilometa 75 mara baada ya upembuzi yakinifu pamoja na ya mchepuko kuingia Kituo cha Mwendokasi Ving’awe hapo Godegode na hatimaye kuunganishwa na barabara ya Iringa-Dodoma.

Akielezea ujenzi huo, Meneja wa TARURA Wilaya ya Mpwapwa, Emmanuel Lukumay alisema tayari kilometa tatu kati ya kilometa za ahadi ya Rais Magufuli kujenga barabara za mjini zimeshakamilika na zilizobaki ujenzi unaendelea.

Naye Meneja wa Tanroads Wilaya ya Mpwapwa, Salome Kabunda alisema tayari wameshajenga kilometa mbili kati ya tano ambazo wanatakiwa kujenga katika barabara itokayo Mpwapwa kwenda Kongwa ambayo itagharimu Sh bilioni 4.9.

Kabunda alisema gharama hizo ni kubwa kutokana na ukweli kwamba barabara hiyo ambayo ilikuwa ikikumbwa na mafuriko mara kwa mara, itainuliwa tuta juu mita tatu, itajengwa madaraja makubwa sita na mengine madogo.

Dkt. Mahenge baada ya kukagua barabara za mjini, kwanza alipongeza juhudi zilizofanywa na Tarura kwa gharama ya Sh milioni 907 kwa ajili ya kujenga barabara za mjini ambayo ni ahadi ya Rais Magufuli na imetekelezwa ndani ya muda mfupi kwa vitendo.

Kuhusu daraja la Miembeni lililosombwa na mafuriko, Lukumay alisema tayari wanatafiti aina ya udongo wa eneo hilo kwa kutumia watalaamu wa Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) hivyo wanachunguza ili kujipanga kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa gharama ya sh milioni 500.

Kwa upande wa Tanroads, Dkt. Mahenge aliwapongeza kwa kuanza ujenzi wa barabara ya Mpwapwa-Kongwa kwa kiwango cha lami ambayo ilikuwa mara kwa mara inakatika kwa mafuriko ya maji.

Dkt. Mahenge alimpongeza Rais Magufuli kwamba amekuwa akiahidi na kutekeleza ahadi zake katika kipindi kifupi, ametoa fedha na sasa barabara hizo zinajengwa kwa kiwango cha lami na kuunganisha wilaya hiyo na barabara kubwa za Dodoma-Morogoro na Iringa-Dodoma kwa kiwango cha lami.

Wilaya ya Mpwapwa ndiyo Kongwe pamoja na Kondoa, lakini ndiyo wilaya pekee ambayo ilikuwa haijaunganishwa na barabara za lami, lakini katika awamu ya tano wilaya hiyo itafunguka kwa kuwa na lami na kuuganishwa na barabara kuu kupitia Kongwa na Jimbo la Kibakwe barabara kuu ya Iringa-Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge (wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri (wa kwanza kulia) wakimsikiliza Mhandisi (wa kwanza kushoto) akisoma taarifa maendeleo ya kazi ya ujenzi wa barabara Mpwapwa.


Picha za matukio ya ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge alipotembelea Wilaya ya Mpwapwa kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.