• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

ALAT yaivulia kofia Dodoma Jiji kwa miradi ya maendeleo

Imewekwa tarehe: June 23rd, 2022

Na. Shaban Ally, Dodoma 

Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) ikiongozwa na mwenyekiti wake, Murshid Ngeze aipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kutekeleza mradi mkubwa wa kimkakati wa soko la kuu la machinga.

Pongezi hizo alizitoa alipofanya ziara ya kutembelea mradi huo ambapo aliongozana na uongozi wa halmashauri hiyo pamoja na wajumbe wa ALAT Taifa.

Ngeze alipata wasaa wa kuzungumzia jinsi alivyovutiwa na ujenzi huo wa soko la machinga ambao umegharimu mabilioni ya fedha ambazo kwa kiasi kikubwa umejengwa kupitia mapato ya ndani yanayokusanywa na Halmashauri ya jiji hilo. Ambapo kwa kiasi kikubwa mwenyekiti alitumia fursa hiyo kutoa pongezi zake za dhati kwa mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Joseph Mafuru pamoja na mkuu wa mkoa, Anthony Mtaka kwa kufanya Dodoma izidi kung'ara.

 "Kwa niaba ya ALAT, nikushukuru sana mkuu wa wilaya pamoja na viongozi wengine wa jiji kwa kuupiga mwingi. Lakini nikuombe mheshimiwa mkuu wa mkoa kuzingatia suala la usalama katika eneo hili la mradi ili kuepusha usumbufu kwa wafanyabiashara",alisema Ngeze.

Sanjari na hilo, mwenyekiti huyo wa ALAT aliendelea kutoa ushauri kwa uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuzingatia maendeleo ya kiuchumi kwa wafanyabiashara hao kwa kuwapa elimu ya biashara ili kuweza kuwakomboa kiuchumi.

"Nikuombe mheshimiwa mkuu wa mkoa uweke utaratibu wa mafunzo ya biashara kwa wafanyabiashara hao kwa lengo la kumuendeleza mfanyabiashara huyo",aliongeza Ngeze.

Mwenyekiti huyo wa ALAT, Murshid Ngeze alihitimisha kwa kuwaomba viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma hususani wajumbe wa ALAT kwenda kujifunza miradi ya maendeleo katika Halmashauri yake ya Kagera, ambapo hii itapanua mawazo ya kimaendeleo kwa viongozi hao.

Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Emmanuel Chibago alipata fursa ya kutoa maneno machache kuhusu ukuaji wa kasi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambapo alianza kwa kumpongeza mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia halmashauri hiyo kiasi cha fedha kwa lengo la kumalizia mradi wa soko la machinga.

Chibago aliendelea kueleza jinsi Halmashauri ya Jiji la Dodoma linavyopokea wageni kutoka halmashauri nyingine kuja kujifunza kuhusu utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimakakati ambayo kwa kiasi kikubwa huchangia kiasi kikubwa cha mapato Katika halmashauri.

Aidha, naibu meya huyo, alihitimisha kwa kuwaomba viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma pamoja na wale wa ALAT kudumisha umoja na ushirikiano baina yao ili kuchochea maendeleo zaidi.

 "Niwaombe ndugu viongozi wenzangu kwa pamoja tudumishe umoja wetu na ushirikiano kwa kuwa asije akatokea mtu yeyote wa kuvunja umoja wetu",alisema Chibago.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Anthony Mtaka mbele ya wajumbe wa ALAT Taifa akielezea jinsi mkoa wake ulivyojipanga kuzisimamia Halmashauri zake katika kutekeleza miradi ya maendeleo yenye tija kwa wananchi wa mkoa huo.Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri akiongea mbele ya wajumbe wa ALAT Taifa walipotembelea jiji la Dodoma lililopo ndani ya Wilaya ya Dodoma.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru akiongea mbele ya wajumbe wa ALAT Taifa jinsi jiji hilo lilivyojipanga kuhakikisha miradi mikubwa ya kimkakati inavyosimamiwa na kutekelezwa ili kuwa na tija kwa wananchi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.