• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Asilimia 70 ya magonjwa ya mlipuko yanatokana ya uchafu - Dkt. Mutayoba

Imewekwa tarehe: November 16th, 2022

Na. Catherine Sungura, WAF-Dodoma

UDHIBITI wa usafi binafsi na usafi wa mazingira unasaidia kupunguza asilimia sabini (70) ya magonjwa ya milipuko yanayotokana na uchafu ikiwemo Kipindupindu.

Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kinga Dkt. Beatrice Mutayoba mara baada ya kufanya usafi kwenye soko la Bonanza lililopo kata ya Chamwino jijini Dodoma ikiwa ni kuelekea wiki ya usafi wa mazingira na matumizi ya choo yanayofanyika kila mwaka kuanzia Novemba 15-19.

“Usafi wa mazingira unasaidia kupunguza asilimia 70 ya magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu hivyo maofisa afya na watendaji wa kata mnapaswa kusimamia vizuri usafi wa mazingira mita tano (5) kuzunguka maeneo ya watu wanayofanyia kazi, ofisini, mashuleni na kwenye nyumba zao ili kuepuka magonjwa ya mlipuko yanayosababishwa na uchafu." Amesema Dkt. Mutayoba.

Aidha, amesema kufanya usafi kwenye mazingira ya kuishi ni jambo jema na kitu kinachosaidia kudhibiti uchafuzi wa vyanzo vya maji chini ya ardhi pamoja na kudhibiti magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu pamoja na magonjwa mengine yanayosababishwa na uchafu.

Dkt. Mutayoba ameongeza kuwa kila eneo lina mwenyewe hivyo ni vyema kusimamia vizuri ili hata usafi wa mwisho wa mwezi au kila jumamosi uweze kusaidia kupunguza kuharibu mazingira.

“Ni vyema sasa kuweka usimamizi kwenye maeneo ya soko ili kuepuka magonjwa ya mlipuko kama kipundupindu pamoja na kusafisha mitaro ya majitaka." Amesema Dkt. Mutayoba.


Hata hivyo Dkt. Mutayoba amewataka maofisa afya pamoja na viongozi wa mitaa na kata kusimamia ujenzi wa miundombinu ikiwemo ujenzi wa vyoo bora na kuvitumia kwa kuweka miundombinu ya kunawia mikono pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu usafi wa mazingira na usafi binafsi.

Wakati huo huo Dkt. Mutayoba amewataka maofisa afya kusimamia sheria na kanuni za usafi wa mazingira ili kuwadhibiti wale wote wanaojenga kwa kuziba mitaro ya maji kwenye maeneo ya masoko ili kuepuka magonjwa ya milipuko watati wa mvua.

Tukio hili lilihudhuriwa pia na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Prof. Davis Mwamfupe.

Chanzo: wizara_afya (instagram)

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.