• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

BARABARA YA MWANGAZA- KISASA MEDELI KM 10.7 KUODOA FOLENI WILAYA YA DODOMA

Imewekwa tarehe: November 29th, 2023

Na. Prisca Maduhu, TAMBUKARELI

MRADI wa Barabara ya Mwangaza-Kisasa Medeli Kilometa 10.7 kwa kiwango cha lami ni muhimu kwa sababu inagusa kata tatu, ikitoa afueni kwa Barabara kuu ya Dodoma -Morogoro kwa kuwaondolea foleni wananchi wa Wilaya ya Dodoma na kuwaletea maendeleo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa akimkaribisha Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, kukagua barabara hiyo.

Alhaj Shekimweri alisema kuwa barabara hiyo inahudumia kata tatu na kupunguza foleni kwa Barabara ya Dodoma -Morogoro na barabara inayoelekea Chuo Kikuu cha Dodoma ikitokea Jakaya Kikwete Convention Center. “Barabara hii inaongeza thamani ya nyumba 300, inaongeza thamani ya eneo la Mwangaza na eneo la Medeli. Pia ni njia ya mchepuko kuwahi kufika Hospitali ya Benjamini Mkapa na Chuo Kikuu cha Dodoma. Barabara inaongeza thamani kwa eneo la Njedengwa Investment Area lililotengwa kwa ajili ya hoteli za kitalii na taasisi mbalimbali zimeshajenga kama Mfuko wa Barabara na Tume ya Taifa ya Uchaguzi” alisisitiza Alhaj Shekimweri.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Tambukareli, Juma Michael alimshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa barabara hiyo. “Tunamshukuru Rais wa serikali ya awamu ya sita, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea mradi huu mkubwa sana wa barabara kutokana na fedha za tozo ya mafuta. Kwa niaba ya wananchi wa Kata ya Tambukareli tunamshukuru sana. Barabara hii itaongeza kasi ya ukuaji wa maendeleo kwa kuwapunguzia wananchi muda wa kukaa kwenye foleni barabarani” alisema Michael.

Akisoma taarifa ya mradi huo, Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura), Wilaya ya Dodoma, Mhandisi Kasongo Morijo alisema kuwa ujenzi wa Barabara ya Mwangaza-Kisasa Medeli Kilometa 10.7 kwa kiwango cha lami unagharamiwa na serikali kupitia fedha za tozo ya mafuta. “Gharama za mradi ni shilingi 10,397,184,981 chini ya Mkandarasi China Henan International Cooperation Group Co. Ltd (CHICO) kwa muda wa miezi 12” alisema Mhandisi Morijo.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.