• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Baraza la Madiwani lapongeza utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo

Imewekwa tarehe: April 25th, 2019
  • Ndani ya mwaka 1 Jiji limepima viwanja zaidi ya 100,000
  • Viwanja 2005 vimetengwa kumaliza migogoro sugu ya ardhi
  • Awamu ya Kwanza Kata ya Ipagala na Makulu vimetengwa viwanja 600 kila Kata, Chang’ombe 200, Nkuhungu 286
  • DC, Mkurugenzi kufanya ziara kusikiliza kero za Wananchi

BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma limekutana leo Aprili 25, 2019 na kujadili utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya tatu (Januari mpaka Machi, 2019) kwa mwaka wa fedha 2018/2019, huku kikihudhuriwa pia na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri hiyo, Watendaji wa Kata, na Wananchi.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Maendeleo katika robo ya tatu, Katibu wa Baraza hilo ambaye pia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Godwin Kunambi alisema kuwa, Halmashauri hiyo kupitia Idara ya Mipango Miji, Ardhi na Maliasili imepunguza kwa kiasi kikubwa migogoro sugu ya ardhi, na kwamba Jiji kwa kushirikiana na wadau wengine wanaendelea kutekeleza majukumu ya Upangaji, Upimaji na uthamini wa ardhi.  

‘Kwa kipindi cha mwaka mmoja, Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeweza kupima viwanja zaidi ya laki moja, tofauti na iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) ambayo kwa miaka yote ilipima viwanja elfu 69 tu, na kati ya viwanja hivyo tulivyopima tumetenga viwanja zaidi ya 2000 kwa ajili ya kumaliza kabisa migogoro ya ardhi katika Jiji la Dodoma’ Alisema Kunambi.

Kunambi alisema kuwa, endapo Halmashauri hiyo ingeviuza viwanja hivyo kwa gharama nafuu kabisa, Jiji lingeweza kupata mapato ya zaidi ya  shilingi Bilioni 1.9, fedha ambazo zingeweza kutumika kujengea Shule, Zahanati na kuboresha huduma nyingine za Jamii.

"Kuna baadhi ya maeneo wananchi wamepewa maeneo bure kwa kulipishwa ada ndogo tu za kisheria, pesa ambayo  inakwenda moja kwa moja Serikali Kuu na kuna maeneo mengine wananchi wanalipia kidogo sana, wapo wananchi waliokaa kwenye maeneo ya shule, maeneo ya wazi na hifadhi za barabara, ambapo ili wananchi hao wapishe maeneo hayo ya Serikali tunahitaji viwanja 1170 kwenye kata ya Ipagala pekee kwa ajili kuwapa kama mbadala, ila kwa awamu ya kwanza tumetenga viwanja 600, Makulu 600, Chang’ombe 200 , Nkuhungu 286, na maeneo mengine tumefanya hivyo...kwa kufanya hivyo, tunaamini tunaweza kumaliza kabisa migogoro ya ardhi katika Halmshauri ya Jiji la Dodoma"  Alisema Kunambi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Dodoma ambaye pia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Antony Mavunde alisema Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeingia katika historia kutokana na kufanikiwa kutatua migogoro mingi ya Ardhi iliyokuwepo kwa muda mrefu.

Mavunde alisema, tangu Mwaka 2015 aliahidi kutatua migogoro ya Ardhi akiwa kama Mbunge na kuhakikisha Wananchi wanauziwa viwanja kwa bei nafuu, jambo ambalo limefanikiwa ambapo sasa wakazi wa Dodoma wanaweza kupata viwanja kwa gharama nafuu ambayo si rahisi kupata sehemu nyingine.

Wakichangia taarifa ya Katibu, Madiwani wengi waliopata nafasi walimpongeza Mkurugenzi wa Jiji Kunambi, Menejimenti na Wafanyakazi wote wa Halmashauri kwa jitihada madhubuti wanazozifanya kwani zimechangia kufanya vema katka ukusanyaji wa mapato na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa na Jiji kwa wananchi wake, huku wakisifu ushirikiano mzuri uliopo kati ya Madiwani na Watendaji wa Halmashauri na kusisitiza ushirikiano na umoja huu uendelee kwa maslahi mapana ya Halmashauri na ustawi wa watu wa Jiji la Dodoma kwa ujumla.

Wajumbe wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakifuatilia Mkutano wa Baraza hilo lililokutana Aprili 25 Mwaka huu kujadili taarifa za utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2018/2019. Kutoka kushoto ni Diwani wa Viti Maalum Mhe. Elisi Kitendya, Diwani wa Viti Maalum Mhe. Joan Mazanda (Katikati) na Diwani wa Kata ya Zuzu Mhe. Awadhi Abdallah.

 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.