• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Baraza la wafanyakazi lafanya kikao kujadili bajeti

Imewekwa tarehe: January 17th, 2025

Na. Coletha Charles, DODOMA

Baraza la Wafanyakazi Halmashauri ya Jiji la Dodoma limefanya kikao maalum kwa ajili ya kupitia bajeti ya mpango wa makisio ya mapato na matumizi ya mwaka 2025/2026, ambayo imeongezeka kwa asilimia 7.04 ukilinganisha na bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025.

Kikao hiko kilifanyika katika ukumbi mkubwa wa mikutano wa Halmashauri Jiji hilo, ambacho kililenga mapendekezo ya rasimu ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 na kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo kwa kuzingatia miongozo ya dira ya maendeleo ya taifa 2025, mpango wa maendeleo wa miaka 5, sheria ya bajeti na. 11 ya mwaka 2015 na malengo endelevu ya maendekeo (SDGs).

Akiwasilisha rasimu ya mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026, Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Francis Kaunda, alibainisha kuwa halmashauri ipo kwenye kundi la utengaji wa fedha kwa asilimia 70 ya mapato yasiyolindwa kwenda kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 30 kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Alisema kuwa miradi ya maendeleo 70% sawa na shilingi bilioni 30.1, matumizi ya kawaida 30% sawa na shilingi 12.9, wanawake, vijana na watu wenye ulemavu 10% shilingi bilioni 4.3, barabara 10% shilingi bilioni 4.3, miradi viporo shilingi bilioni 7, miradi mikakati shilingi bilioni 5, miradi ya kipekee shilingi bilioni 1, miradi ya kata shilingi bilioni 6.1 na vipaumbele vingine vya divisheni shilingi 2.3.

“Kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji, naomba kutamka rasmi kuwa rasimu ya makisio ya mpango na bajeti ya Halmshauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2025/26 ni jumla ya shilingi bilioni 147.9, kati ya fedha hizo shilingi bilioni 67.3 ni mapato ya ndani, shilingi bilioni 65.7 ruzuku ya mishahara, shilingi bilioni 3 ruzuku ya matumizi mengineyo na shilingi bilioni 11.7 ruzuku ya miradi ya maendeleo”.

Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, pia aliwasilisha mapitio ya bajeti ya nusu mwaka wa fedha 2024/25, ambapo alisema Halmshauri ya Jiji la Dodoma iliidhinishiwa bajeti ya shilingi bilioni 143.1 hadi kufikia desemba 2024, jumla ya shilingi bilioni 76.1 zilikusanywa sawa na 53.2% ya makisio.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.