• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Benki ya Dunia yapongeza miradi ya Kimkakati - Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: December 8th, 2018

BENKI ya Dunia kupitia kwa Wataalamu wake wa ushauri na tathimini wamepongeza utaratibu unaotumiwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kusimamia ujenzi wa miradi mikubwa na kuweka mazingira rafiki na mahusiano mazuri baina ya Wakandarasi na Wananchi kwenye hatua za Uendelezaji wa Miji ya Kimkakati (TSCP) katika Jiji la Dodoma, ikiwa ni pamoja na mradi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Kisasa na Soko Kuu katika eneo la Nzuguni Jijini humo.

Haya yamebainishwa na ujumbe wa wataalamu washauri na tathimini ya maendeleo ya Ujenzi kwa kushirikiana na wasimamizi wa miradi ya Uendelezaji wa Miji ya Kimkakati (TSCP) kutoka TAMISEMI katika ziara ya siku mbili ya kutembelea miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Benki ya Dunia ili kuona hatua iliyofikiwa kwa kuzingatia muda wa ujenzi na masharti ya ujenzi yaliyoafikiwa kwenye mikataba.

“Kwa kweli katika miradi tuliyotembelea nchi nzima, Jiji la Dodoma mmetufurahisha sana, mmeonyesha mshikamano wa pamoja katika usimamizi na ndiyo maana mmefanikiwa kutatua changamoto kwa kiasi kikubwa” alisema Beatrice Mchome ambaye ni Afisa Mazingira na Mshauri wa Masuala ya Kijamii kutoka TAMISEMI.

Mratibu wa Uendelezaji Miji ya Kimkakati Jiji la Dodoma, Mhandisi Emmanuel Manyanga amesema Serikali imesaini mikataba ya ujenzi wa miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Benki ya Dunia na kwamba kuna miradi mikubwa inayoendelea kujengwa ikiwemo Kituo Kikuu cha mabasi, Soko Kuu, Kituo cha maegesho ya malori, Barabara za Lami za mitaa, vivuko vya waenda kwa miguu, Bustani ya mapumziko na burudani, pamoja vizimba katika maeneo ya kukusanyia takangumu.

Manyanga alisema miradi mingine ni ujenzi wa Mtandao wa barabara katika mitaa mbalimbali zenye urefu wa kilometa 26.7 kwa kiwango cha lami, ufungaji wa taa za barabarani zitakazotumia mwanga wa jua, na ujenzi wa mtaro mkubwa wa maji ya mvua wenye urefu wa kilometam 6.5 katika eneo la Ilazo – Ipagala.  

“Benki ya Dunia huleta wataalamu kukagua miradi inayojengwa kwa uwiano na fedha walizotoa kugharamia miradi hiyo na kuangalia Maendeleo, Changamoto, Kushauri pale inapobidi na kuangalia mapungufu ili kuongeza ufadhili katika miradi husika.” alisema Mayanga

Miradi iliyotembelewa na Ujumbe huo kutoka Benki ya Dunia na Wizara ya TAMISEMI ni pamoja na Soko Kuu la Kisasa, na Kituo Kikuu cha mabasi inayojengwa na Mkandarasi wa Kitanzania kupitia kampuni ya Mohamed Builders Ltd eneo la Nzuguni, Ujenzi wa Bustani ya Mapumziko na burudani linalojulikana kama ‘Chinangali Park’ na Dampo la Kisasa la kuhifadhi takangumu kwa teknolojia ya kuzika ardhini (Sanitary Landfill) lililopo eneo la Chidaya nje kidogo ya Jiji.

Miradi yote imenza kujengwa Julai Mosi Mwaka 2018, ikiwa ya thamani ya shilingi bilioni 77.8 za Kitanzania na inatarajiwa kukamilika Mwezi Oktoba, 2019.

 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.