• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Bil. 83.1 zatumika utekelezaji wa mradi wa uendelevu SRWSS

Imewekwa tarehe: July 21st, 2024

Mratibu wa Mradi wa Uendelevu wa Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (SRWSS) kutoka TAMISEMI Bw. Seleman Yondu amesema mradi huo ukwa mwaka wa fedha wa 2023/2024 umepokea jumla ya Tsh. 83.1Bil kwa ajili ya utekelezaji wake huku eneo la Afya ikitumia shilingi Bil. 54.39 na ujenzi wa miundombinu ya Elimu ikitumia shilingi Bil. 28.73

Amesema, Mradi unatekelezwa katika mikoa yote 25 ya Tanzania bara na Halmashauri 137, huku akiweka bayana kuwa Manispaa, miji na majiji sio sehemu ya mradi huu.

Yondu ameyasema hayo Julai 17,2024 wakati wa kikao kazi kilichofanyika mkoani Morogoro kikiwahusisha waganga Wakuu wa Mikoa na Maafisa Afya wa Mikoa yote Tanzania Bara lengo likiwa ni kujitathmini juu ya utekelezaji wa Mradi huo.

Amesema mpaka sasa mradi wa SRWSS umefikia vituo vya kutolea huduma za Afya 2,727 na shule za Msingi 1,842, kwa mwaka wa fedha 2023/24 jumla ya vituo vya kutolea huduma za Afya 838 na shule 566 vimepokea fedha za utekelezaji.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Anyantike Mwakitalima amesema mradi huo umefanyika kwa mafanikio hususan ukilinganisha malengo na kazi iliyofanyika huku akibainisha kigezo kimojawapo kuwa kaya zenye watu zaidi ya 10,000zimefikiwa na kutoa elimu ya kuwa na vyoo bora na kuvitumia huku lengo likiwa ni kuzifikia kaya zenye watu 9,000.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Best Magoma ameishukuru Serikali kwa kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za Afya ameiomba Serikali usafiri wa pikipiki kwa ajili ya watendaji wakutoa huduma za Afya ngazi ya chini ili kuwawezesha watendaji hao kufika kila kaya na kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Naye Afisa Afya Mkoa wa Morogoro Bi. Prisca Laurent kwa niaba ya washiriki wengine amesema kufanya vizuri katika mradi huo utapunguza magonjwa ya mlipuko lakini pia kuziwezesha Halmashauri kupewa fedha zaidi.

Aidha, amebainisha kuwa uhamasishaji wa kujenga na kutumia vyoo bora kwa wananchi wa Mkoa huo umeongezeka kutoka asilimia 72 hadi 73 na kwamba Mkoa huo kuanzia mwaka 2023 tayari umepokea zaidi ya Tsh. 3 Bil. Kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.