• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Bilioni 3.6 kukarabati shule za Jiji

Imewekwa tarehe: August 6th, 2021

Na Getruda Shomi, DODOMA.

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetenga shilingi bilioni 3.6 kwa ajili ya kukarabati shule zilizopo kwenye Halmashauri hiyo ikiwa ni moja ya mpango wake wa kufanya maboresho ya kimiundombinu katika shule hizo ili kuendelea kuimarisha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Joseph Mafuru wakati akijibu swali la papo kwa papo lililoulizwa na Diwani wa Kata ya Makole Mhe. Omary Haji katika kikao cha robo ya nne cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika Chuo cha Mipango.

Mkurugenzi Mafuru alisema kuwa ameshatoa maelekezo kwa Maafisa Elimu wa shule za msingi na sekondari kuanza mchakato wa manunuzi na kutafuta mafundi ili kuweza kukarabati shule hizo.

“Jiji limetenga zaidi ya shilingi bilioni 3.6 kwa ajili ya shule zake, kila shule iliyoingizwa kwenye bajeti itaboreshwa, nimeshatoa maelekezo kwa Afisa elimu shule ya sekondari na msingi waanze mchakato wa kuwatafuta mafundi, hivyo kama Makole ipo kwenye bajeti itafanyiwa kazi.” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Aidha, alisema kuwa kwa shule ambazo hazikuwekwa kwenye bajeti hiyo ya ukarabati zitatakiwa kufanyiwa kazi kwa kushirikisha na wadau wa maendeleo Jiji la Dodoma kwani wamekuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya Jiji hilo. 

Ameongeza kuwa utekelezaji wa mkakati huo wa kukarabati shule za msingi na sekondari utaanza mwezi Agosti, 2021 ambapo bajeti ipo tayari na utekelezaji wake utaanza hivi karibuni huku akitoa wito kwa Madiwani kutoa ushirikiano wakutosha kipindi cha utekelezaji wa mradi huo.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mafuru alijibu swali la Diwani wa kata ya Mbabala Mhe. Paskazia Mayala lililouliza Halmashauri amejipanga vipi kutoa elimu ya chanjo katika Kata za pembezoni, ambapo alijibu kuwa ”timu ya Madaktari na Wataalam wa afya itatembea kwenye Kata na maeneo yote yenye mikusanyiko ili kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kwa kina kwa sababu upotoshaji ni mwingi na Halmashauri inatambua uwepo wa changamoto hiyo.

Diwani wa Kata ya Makole Mhe. Omary Haji na waheshimiwa madiwani wengine wa Jiji la Dodoma wakifuatilia hoja zilizokuwa zikiwasilishwa katika Baraza la Madiwani la Jiji la Dodoma.


Wajumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Jiji la Dodoma, Mhe. Jaffar Mwanyemba (kushoto), Mhe. Beatrice Ngerangera (katikati) na Mhe. Gideon Nkana (kushoto) kwa makini wakifuatilia mada wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mhe. Awadh Abdallah wa Kata ya Zuzu na Mhe. Amos Mbalanga wa Kata ya Kiwanja cha Ndege wakiwa kwenye kikao cha Baraza la Jiji la Dodoma.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang'anya ambaye ni Mkurugenzi mteule wa Halmashauri ya Njombe (kushoto) na Mkuu wa Idara ya Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji wa Jiji la Dodoma, Shabani Juma ambaye ni Mkurugenzi mteule wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika (kulia) wakiteta jambo na Mkuu wa Kitengo cha Uchaguzi wa Jiji la Dodoma, Albert Kasoga.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.