• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Bima ya Afya kwa familia ina faida - DC Katambi

Imewekwa tarehe: July 10th, 2019

MFUKO wa Afya ya Jamii Ulioboreshwa unalenga kumhakikishia mwananchi uhakika wa afya njema kupitia matibabu kwa mwaka mzima wilayani Dodoma.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Patrobas Katambi alipokuwa akizindua kampeni ya uhamasishaji mkubwa wa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa jana katika mtaa wa Mahomanyika katika kata ya Nzuguni jijini Dodoma.

Katambi alisema kuwa watu wengi wanatembea na magonjwa sababu hawaendi hospitali kupima kwa kuogopa kutozwa fedha. “Siku ugonjwa ukizidi utakuta huwezi kwenda kufanya kazi na kutafuta fedha na wala huwezi kutibiwa. Nataka kuwaambia ukiwa na bima ya afya kwa familia ya watu sita unafaida mara mia nane tofauti na mtu asiyekuwa na bima hiyo. Huku ukienda tu hospitali unalipa shilingi 6,000 ukipewa rufaa ya kwenda mjini unalipa shilingi 15,000” alisema Katambi.

Mkuu wa Wilaya aliwakumbusha wananchi kuwa Rais Dkt. John Magufuli wakati akiomba kura alisema kuwa ataboresha huduma za afya. Miongoni mwa utekelezaji wa ahadi hiyo ni uboreshaji wa huduma za CHF ambapo unalipia shilingi 30,000 na kuhudumiwa watu sita kwa mwaka mzima. Katika kuonesha serikali inawajali wananchi wake, kila anayelipia shilingi 30,000 kwa CHF serikali inaongeza tena shilingi 30,000.

Akiongelea faida za CHF iliyoboreshwa, Katambi alisema kuwa inamuwezesha mwananchi kupata huduma bora katika eneo lake. “Serikali imeendelea kujenga na kuboresha zahanati, vituo vya afya na hospitali na kulipa mishahara madaktari na wataalam wa sekta ya afya ili wananchi waweze kupata huduma bora” alisema Katambi. Faida nyingine ya CHF aliitaja kuwa ni upatikanaji wa vifaa tiba katika vituo vya afya vilivyopo katika maeneo yao.

“Ndugu zangu, napenda kuwahakikishia kuwa ukiwa na bima ya afya unakuwa umejiandaa muda wowote katika eneo la matibabu. Niwaombe wananchi wa Mahomanyika tujisajili katika bima ya afya. Huna sababu ya kukopa unapougua au kuuguliwa, tujipange sasa” alisisitiza Katambi.

Awali mratibu wa CHF katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Patrick Sebyiga alisema kuwa lengo la maboresho ya CHF ni kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanajiunga na mfuko huo ambao utawasaidia kupata huduma za afya kwa gharama nafuu.

Mratibu huyo alisema kuwa dhumuni la kuboresha CHF ni kutenganisha watoa huduma za tiba na usimamizi wa bima, kuweka mfumo wa bima, kuongeza idadi ya wananchama, kutoa mfumo wa utambulisho utakaowezesha huduma kupatikana kwa mwanachama akiwa sehemu yeyote katika Mkoa wa Dodoma.  

CHF iliyoboreshwa imebuniwa na wataalam wa mradi wa HPSS- Tuimarishe afya ikiwa imetumia uzoefu wa mifuko ya bima ya afya ya jamii kutoka India pamoja na matokeo ya tafiti zilizofanywa ndani na nje ya nchi.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Patrobas Katambi (mwenye kipaza sauti) akiongea na wananchi wa Mahomanyika alipokuwa akihamasisha jamii kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.