• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Bura: Wanawake tuache utegemezi

Imewekwa tarehe: March 8th, 2020

MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Dodoma kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Felista Bura amewataka wanawake nchini kushiriki katika shughuli zitakazowezesha kujipatia kipato, huku akiwasisitiza kuachana na dhana ya kuwategemea wanaume kwa kila kitu katika kujipatia mahitaji yao ili kuweza kujenga jamii imara na yenye maendeleo.

Aliyasema hayo wakati akitoa hotuba katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani Machi 8 mwaka huu yaliyofanyika katika ngazi ya Mkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Mkonze jijini hapo.

Bura alisema kuwa, usawa wa 50-50 kati ya wanawake na wanaume hauwezi kupatikana kama wanawake wataendelea kuwa na dhana ya utegemezi, lakini wakiamua kufanya kazi wataweza kujikwamua na dhana hiyo katika utekelezaji wa kaulimbiu isemayo “kizazi cha usawa kwa Tanzania ya sasa na ya baadae”.

“Kumekuwa na desturi ya wanawake kutokufanya shughuli za kujiingizia kipato na kutegemea wanaume kutekeleza jukumu hilo, usawa tunaouhitaji tutaupataje wakati hata kazi hatutaki kufanya, wakati umefika sasa wa wanawake kubadilika, kundi hili la wanawake ambao wanaishi hivi wanatuharibia malengo yetu ya kujikwamua kiuchumi, tunaendelea kudharaulika na kuonekana hatuwezi kwa ajili yao.

“Wakati umefika sasa wa wanawake kufanya maendeleo kwa kutumia kipato chetu wenyewe, upendeze kwa hela yako mwenyewe, usimtegemee mumeo kwa kila kitu, fanya bidii katika kujipambania na kujiwezesha mwenyewe usisubiri hadi uwezeshwe, hautaweza kujikomboa kuendea usawa endapo hata mahitaji yako mwenyewe unashindwa kujitimizia unasubiri hadi ufikiriwe na mtu mwingine,” alisema Bura.

Mbunge huyo pia aliitaka jamii kuondokana na mila kandamizi ikiwemo tabia ya wanaume kuchukua pesa zote baada ya mavuno kwa kushirikiana na wake zao kwa madai kuwa wao ndiyo vichwa na mihimili ya familia hivyo wana haki ya kuamua chochote wakati wowote.

“Kuna tabia pia kwa wanaume, ambao wanatumia kama silaha kumdidimiza mwanamke kwa kuwa tu amepewa nguvu na mila na desturi, kuna wanawake wanafanya kazi mno lakini hawafaidi matunda ya kile wanachokifanya, baada ya mafanikio wanaume ndo watu wanofanya starehe na kufuja mali bila hata kuwapa wanawake waliotafuta pamoja, tabia hizi zikomeshwe, wanawake wapatiwe stahiki zao kama wafanyavyo kazi.

“Nawashauri wanawake wenzangu, tuanzishe miradi itakayotuibua kiuchumi, kwani tutakuwa tumeshaondokana na vyote vinavyotukwamisha kimaendeleo, kuna mikopo ya Halmashauri tuunde vikundi tuwezeshwe kupitia asilimia nne ya mikopo hii tujiinua wenyewe kiuchumi”, alisema mbunge huyo.

Mwaka wa fedha 2018/2019, Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilikopesha jumla ya zaidi shilingi Bilioni 1.825 kwa vikundi 353 vya wanawake, ikiwa ni  utekelezaji wa agizo la Serikali Kuu la kila asilimia nne ya mapato ya ndani ya kila Halmashauri kuwapatia mikopo isiyo na riba wanawake.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.