• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Bwawa wa Zuzu laanza kuleta manufaa

Imewekwa tarehe: August 29th, 2021

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KAMATI ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma imefurahi kuona wakazi wa Kata ya Zuzu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakinufaika na shughuli za uvuvi katika bwawa la Zuzu.

Akielezea thathimini ya Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Dodoma baada ya kutembelea bwawa hilo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Meja Mst. Johnick Risasi alisema kuwa kamati yake imefurahia kuona wakazi wa Kata ya Zuzu wakinufaika na bwawa hilo. Aidha, aliishauri halmashauri kufanya utafiti wa jinsi ya kuliendeleza bwawa hilo ili liwe na tija zaidi kwa wananchi na kuiwezesha halmashauri kupata mapato pia.

Nae Katibu wa CCM Wilaya ya Dodoma, Sophia Kibaba alishauri kuwa kina cha bwawa hilo kiongezwe ili kuongeza uhakika wa upatikanaji Samaki. “Mwenyekiti, nashauri kuongeza kina cha bwawa la Zuzu ili kupata samaki wengi zaidi. Upatikanaji wa samaki wengi utapunguza kuagiza samaki kutoka nje ya Dodoma na kupunguza gharama kwa wananchi wetu, wakati huohuo kuwahakikishia mlo bora na kukabiliana na changamoto ya lishe” alisema Kibaba.

Akiwasilisha taarifa ya bwawa la Zuzu, Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Gratian Mwesiga alisema kuwa bwawa hilo ni muhimu. “Bwawa hili lilianza kama mbuga kwa miaka mingi ambapo wakazi wa maeneo jirani walilitumia kulima Mpunga. Zamani kwenye mbuga hii kulikuwa na miti mingi hivyo maji yalikuwa yanatuama na kukauka. Baadae wananchi walikata miti yote na kuendelea kulima Mpunga. Baada ya kukata miti, maji hayakuendelea kutuama kwa muda mrefu, yalijaa wakati wa mvua na baadae kukauka” alisema Mwesiga.

Mkuu huyo wa idara alisema kuwa bwawa hilo lina jumla ya wavuvi 15 na wote wamelipa leseni ya uvuvi kwa mwaka 2021. “Samaki wanaopatikana kwenye bwawa hili ni Kambale na Perege” alisema Mwesiga.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa uvuvi katika bwawa hilo, Omary Kagusa alisema kuwa vijana katika kata hiyo hawakuwa na elimu ya uvuvi wa kutumia mitumbwi. Alisema kuwa walisaidiwa kupata elimu hiyo kwa kushirikiana na wataalam wa uvuvi kutoka maeneo mengine.

Mwenyekiti wa CCM Dodoma Mjini, Meja Mst. Johnick Risasi (mwenye shati la kijani) na mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Rukia Bakari (kushoto) wakimsikiliza Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Gratian Mwesiga akitoa maelezo huu ya bwana na shughuli za uvuvi katika bwawa la Zuzu wakati Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Dodoma ilipofanya ziara katika Kata ya Zuzu.

Mwenyekiti wa CCM Dodoma Mjini, Meja Mst. Johnick Risasi (kushoto) akitoa nasaha zake mbele ya wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Dodoma na wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakati kamati hiyo ilipotembelea na kukagua miradi katika Kata ya Zuzu Jijini Dodoma mwishoni mwa wiki.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.