• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

CCM Chang'ombe yafurahishwa utendaji kazi wa Diwani Fundikila

Imewekwa tarehe: September 3rd, 2023

Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe kimefurahishwa na jinsi diwani wa kata hiyo anavyohamasisha na kushiriki katika shughuli za maendeleo na kuifanya kuwa ya kuigwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chang’ombe, Bashiri Iddy alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa wa Chilewa katika Kata ya Chang’ombe kwenye mkutano wa hadhara.

Iddy alisema “tunaposema Diwani wa kata hii Bakari Fundikila anafanya kazi katika kata yake kwa weledi na uaminifu tuendelee kumuamini tunamaanisha tumeridhishwa na utendaji kazi wake. Leo tunavyosema amefanya kazi ya ujenzi wa kituo cha Polisi, amefanya kazi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe, amefanya kazi ya ujenzi wa masoko mawili Soko la Mavunde na lile la Hamvu, amefanya kazi ya kufungua barabara, amefanya kazi ya kuboresha elimu katika shule zetu siyo tunatania. Ni kazi ambazo kila mmoja wetu anaziona na anaweza kuzielezea. Kile kituo cha Polisi kinachojengwa pale ukubwa, ubora, sifa na uwezo kwa kituo hicho tunaongelea jitihada za Diwani Fundikila”.

“CCM Kata ya Chang’ombe tunasema Diwani Fundikila anakuwa ni kijana wa mfano, anakuwa ni kiongozi wa mfano. Leo kwa ubora wa utendaji kazi wake, Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuna nafasi inahitaji watu watatu makini na katika wale watu watatu yeye ni mmoja wao. Kwa nini ni mmoja wao hii ni kwasababu ya ubora na kazi anazofanya katika kata yake” alisema Iddy kwa kujiamini.

Mwenyekiti huyo alipongeza ushirikiano baina wenyeviti wa mitaa na diwani. “Ushirikiano wenu unanipa ujasiri na nafasi ya kuwatetea kwa jinsi mnavyofanya kazi. Hata mkichukua fomu nikiwa nikiwepo nitazipigania. Sitakubali kufanya mabadiliko ya viongozi kwa sifa za akili za kupenda watu, yaani unampenda mtu kwa sababu anajua kuongea na anajua kucheka lakini kwenye kazi hakuna kitu” alisema Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chang’ombe.

Chama cha Mapinduzi Kata ya Chang’ombe kinafanya ziara ya kikazi katika Matawi yote ya chama hicho kukagua uhai wa chama, utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, kusikiliza kero za wananchi na kuwashukuru wanachama wake kwa kuchagua uongozi wa CCM Kata ya Chang’ombe.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.