• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

CCM Dodoma walipongeza Jiji ujenzi wa jengo la 'Machinga'

Imewekwa tarehe: January 16th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepongezwa kwa ujenzi wa jengo la kisasa la wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) ili waweze kufanya shughuli zao katika eneo rasmi na salama.

Pongezi hizo zilitolewa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma, Pili Mbanga wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la kisasa la Machinga jijini Dodoma tarehe 13 Januari, 2022.

Mbanga alisema “pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwa ushauri kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mkuu wa Mkoa aliona Machinga wanatakiwa kuwa katika eneo zuri. Pongezi kwa Mkurugenzi wa Jiji kwa kutoa fedha nyingi kujenga jengo la Machinga ili wafanye kazi kwa staha”.

Aidha, aliwataka Machinga kuwa wazalendo kwa halmashauri yao na serikali yao kwa ujumla. “Tunatamani kuona Machinga wanatoka katika umachinga na kuwa wafanyabiashara wakubwa. CCM tutaendelea kuunga mkono juhudi za Rais na Serikali kwa ujumla. Rai kwa wilaya nyingine katika Mkoa wa Dodoma kuwatafutia Machinga maeneo mazuri ya kufanyia shughuli zao” alisema Mbanga.

Naibu Meya, Emmanuel Chibago alitoa pongezi kwa Mkuu wa Mkoa na ofisi yake kuendelea kuliunga mkono Jiji la Dodoma. “Hii inalifanya Baraza la Madiwani kuwa makini kumuunga mkono Rais kwa kuhakikisha Machinga wanafanya shughuli zao katika maeneo rafiki. Kwa niaba ya madiwani tupo pamoja” alisema Naibu Meya Chibago. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa Dodoma, Bruno Mponzile alisema kuwa Machinga wameshirikishwa katika mchakato wa utafutaji wa eneo na ujenzi wa jengo la kisasa la Machinga. “Rai yangu, Machinga tuwe wazalendo kwa nchi yetu, tusiingize watu wasiohusika katika mradi huu. Tukibaini anayetaka kuvuruga mpango huu hatutamvumilia. Walengwa ni wale Machinga 3,313 tuliowasajili.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alifanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la kisasa la Machinga akiambatana na Katibu Tawala Mkoa, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, viongozi wa Chama cha Mapinduzi na maafisa waandamizi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.