• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

CD MAFURU: Gharama kupimiwa sasa 120,000, Jiji lashusha vifaa vyake kwa milioni 240

Imewekwa tarehe: January 31st, 2022

MKURUGENZI wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru amesema kuwa kupatikana kwa vifaa vipya vya kisasa vya upimaji ardhi kwenye halmashauri hiyo, kuanzia sasa hawataingia tena mikataba na makampuni binafsi ya upimaji ardhi.

Mafuru alisema hayo wakati wa kupokea na kuzindua vifaa hivyo vya kisasa vya upimaji ardhi vilivyonunuliwa kwa gharama ya shilingi milioni 240 kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Alisema kuwa baada ya Jiji kupata vifaa vyake gharama za upimaji itakuwa Sh 120,000 tu ambapo awali gharama za upimaji kwa makampuni binafsi ya upimaji ilikuwa ni shilingi 250,000.

Aidha, Mafuru alisema kuwa baada ya upatikanaji wa vifaa hivyo ni mategemeo yao sasa kutoingia mikataba na makampuni binafsi ya upimaji ardhi na makampuni yanayoendelea na kazi hiyo mara baada ya kazi zao kumalizia itakuwa imekwisha.

"Makampuni binafsi yamekuwa yakilalamikiwa na kusababisha migogoro mingine ya ardhi na lawama kutupiwa halmashauri ya jiji. Viwanja vilikuwa vinagawanywa vidogo vidogo, ili kuongeza faida na kwenye maeneo mengi kulikuwa kunaibuka migogoro kila siku." alisema Mafuru

Aliongeza kuwa awali Jiji lilikuwa na mahitaji makubwa ya upimaji viwanja na lisingeweza kufanya kazi hiyo peke yake ndipo wakaalika makampuni binafsi, lakini mwisho wa siku walizalisha migogoro mingine na Halmashauri kunyooshewa vidole.

Alisema walikuwa na mikakati mingi ya kuimarisha shughuli za upimaji ardhi na mwaka 2019 walinunua magari matatu na mwaka 2020 walinunua tena magari matatu.

Kwa uwepo wa vifaa hivi, sasa tunauwezo wa kupima viwanja 300 kwa siku na tutakwenda kupima maeneo ambayo upimaji ulisimama kwenye maeneo mbalimbali ndani ya halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Aliyataja maeneo hayo kuwa ni Bihawana, Gawaye, Hombolo na maeneo mengine ya pembezoni ambayo upimaji ulisimama. Upimaji huo utafanyika kwa gharama nafuu.

Akifafanua zaidi, Mkurugenzi huyo alisema, sasa wako kwenye taratibu za kununua mitambo kwa ajili ya kufungua barabara ili kufanya Dodoma kuwa mji uliopangwa kuliko miji yote.

"Tunaenda kufungua barabara na kufanya mapinduzi makubwa kwenye sekta ya ardhi.” Alimalizia Mkurugenzi Mafuru.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Jabir Shekimweri alisema vifaa hivyo kama vitatumika vizuri vitapunguza changamoto.ya upimaji katika maeneo mengi.

Alisema wakati Jiji linakabidhiwa iliyokuwa Mamlaka.ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kulikuwa na mahitaji ya viwanja 20,000 na kufikia sasa kazi kubwa imefanyika. "Jiji kupata seti sita zenye uwezo wa kupima viwanja 300 kwa siku sawa na viwanja 9,000 kwa mwezi ni jambo la kupongezwa," alisema Mkuu huyo wa Wilaya.

"Ufanisi wa utendaji ni matokeo ya vitu vingi, tusijidanganye tukiwa na vifaa vizuri ndio tumemaliza, kwenye Idara ya ardhi sasa wana vifaa vya kutosha kusiwe na kisingizio, tuna uwezo wa kupima viwanja vingi hatutegemei tena migogoro kutoka kwa wananchi," alisema Shekimweri.

Naye Kaimu Mkuu wa idara ya Mipango miji Jiji la Dodoma Amelye Chaula, akitoa taarifa ya upatikanaji wa vifaa hivyo, alisema kuwa hivi sasa itawaondolea gharama ya kulipia makampuni ambayo ilikuwa ikiongezeka kila wakati.

Pia itaondoa malalamiko kutoka kwa wananchi yanayotokana na upimaji wa makampuni ambayo yalikuwa yakipima viwanja vidogo vidogo ili kuongezea faida.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Prof. Davis Mwamfupe akizungumza wakati wa hafla hiyo

Mkurugenzi wa Jiji Joseph Mafuru akizungumza wakati wa hafla hiyo

Baadhi ya wadau wakifuatilia uzinduzi wa vifaa hivyo

 Mkuu wa Wilaya Jabir Shekimweri akipata maelezo ya jinsi vifaa hivyo vinavyofanya kazi kutoka kwa mkuu wa kitengo cha upimaji Enock Katete

Baadhi ya vifaa vya upimaji ardhi vilivyonunuliwa na Jiji kwa gharama ya shilingi milioni 240

Mkuu wa wilaya Jabir Shekimweri akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Halmashauri ya Jiji wakiongozwa na Meya Mstahiki Prof. Davis Mwamfupe na Mkurugenzi wa Jiji Joseph Mafuru baada ya uzinduzi wa vifaa hivyo vya upimaji ardhi 


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.