• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

CD Mafuru: Tunajenga ofisi mpya ya Jiji

Imewekwa tarehe: February 21st, 2022

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetenga Shilingi bilioni saba katika mwaka wa fedha 2022/23 kwa ajili ya kujenga Jengo la Ofisi Kuu ya Jiji inayolingana na hadhi ya Makao makuu ya Serikali.

Jiji limetenga fedha hizo ambazo ni sehemu ya bajeti ya mwaka 2022/23 ya Shilingi bilioni 100.94 ambazo zitakusanywa na kutumika kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ukiwemo huo wa ujenzi wa ofisi kuu ya Jiji hilo.

Akiwasilisha Bajeti ya Jiji kwa Mwaka 2022/23 mbele ya Baraza la Madiwani jijini hapa mwishoni mwa wiki iliyopita, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alisema Jiji limepanga kujenga ofisi bora itakayolingana na hadhi ya Jiji la Dodoma kama makao makuu ya serikali katika eneo la uwekezaji la Njedengwa na ujenzi wake utaanza Julai mwaka huu.

“Jengi la Makao Makuu ya Jiji litajengwa eneo la Njedengwa ambapo ni kati ya Jiji kwa sasa kwani jengo linalotumiwa kwa sasa lilijengwa na CDA mwaka 1973,” alisema.

Mafuru alisema pamoja na mradi huo, Jiji limeweka kipaumbele katika kukamilisha miradi viporo, kuchangia nguvu za wananchi, kujenga miradi ya maendeleo inayoleta tija, kuimarisha seka ya afya, elimu, kilimo na mifugo na kuimarisha utoaji wa huduma katika maeneo ya pembezoni.

Pia bajeti hiyo pia itazingatia stahiki za madiwani, stahiki za watumishi na mazingira mazufuri ya kufanyia kazi.

Akizungumzia bajeti ya mwaka uliotangulia kati ya kipindi cha Julai hadi Desemba alisema mwaka 2021, Shilingi bilioni 13.8 zimetumika katika kutekeleza miradi ya kimakati, upimaji wa ardhi, malipo ya fidia ya ardhi na miradi ya kijamii.

 Pia imetumika katika kujenga mahakama ya jiji, ununuzi wa magari matatu kwa ajili ya kuimarisha ukusanyaji wa mapato na ununuzi wa vifaa vya upimaji ardhi vilivyogharumi Sh milioni 240.

Pia halmashauri imefanikiwa kutoa mikopo kwa vikundi 49 yenye thamani ya Shilingi bilioni 1.04 na kuendelea kukamilisha mradi wa kimkakati wa hoteli inayojulikana kama Dodoma City Hotel.

Pia kuendelea na ujenzi wa miradi ya kimkakati wa kitega uchumi katika mji wa Serikali Mtumba ambacho hadi sasa kimefikia asilimia 90 katika awamu yake ya kwanza.

Halmashauri pia imefanikiwa kufanya uthamini katika maeneo mbalimbali ya Nala, Mtumba, Kikombo na Ihumwa ambapo Shilingi bilioni 1.32 zimelipwa kama fidia kwa wananchi kupitia fedha za ndani.

Katika kipindi hicho Jiji limepima viwanja 10,339 katika maeneo mbalimbali ya Ngh’ongh’ona, Hombolo Bwawani, Zuzu na Mpunguzi. Pia limeandaa mipango 41 ya matumizi bora ya ardhi.

Katika kipindi cha Julai hadi Desemba, mwaka jana, Jiji hilo limetoa jumla ya hati 8,247 kwa wamiliki mbalimbali wa ardhi katika jiji hilo.

Pia limesimamia ujenzi wa madarasa 143 ya shule za sekondari na nne za msi ngi kupitia fedha za Covid-19 ambapo Sh bilioni 2.9 zilimtumika.

Lakini pia Jiji limekamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa 75 za vya shule za msingi na sekondaro kupitia fedha za ndani.

Katika bajeti ya mwaka 2022/23 Jiji linakusudia kukusanya na kutumia bajeti ya Shilingi bilioni 100.9, fedha hizo zitapatikana kupitia mkakati wake wa kukusanya madeni, kutumia vyanzo vya zamani na vipya kama minada.

Pia litahakikisha ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo na vituo vyote unatumia mfumo wa kielektroniki ili kuweza  kudhibiti upotevu wa mapato hayo.

Pia Jiji katika kudhibiti makusanyo, linakusudia kuandaa kanzidata ya viwanja vyote vinavyozalishwa ili kudhibitiutoaji na ulipaji au uendeleaji wa viwanja hivyo.

Pia kufanya tathmini ya madeni ambayo halmashauri inadai tangu zamani hadi sasa ili kuhakikisha Jiji linaongeza mapato.

Linakusudia kuanzisha (SPV) ambayo itasimamia miradi yote ya kimkakati ikiwemo ya Hoteli ya Jiji  Kitega Uchumi cha Halmashauri,  Makazi ya Bei Nafuu, Soko Kuu la Job Ndugai, Kituo Kikuu cha Mabasi na Eneo la Kuegesha Maroli la Nala.

Pia litatumia watendaji wa kata, mitaa na vijana wanaoitwa Rangers pamoja na madiwani kufuatilia tozo, vibali vya ujenzi pamoja na leseni za makazi ili kuhakikisha kodi inakusanywa.

Akizungumza Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikira alisema ajeti inajitoshereleza na Mkurugenzi wa Jiji ametoa ufafanuzi kuhusu vifungu vyote hivyo wanaridhia kuipitisha.

Meya wa Jiji la Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe aliwahoji madiwani kuhusu bajeti hiyo ya 2022/23 na wakadhirika na kuipitisha kwa kauli moja na wakaahidi kwenda kusimamia makusanyo katika kata zao.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.