• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Chama cha AAFP chasifu mchakato wa uteuzi wagombea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Imewekwa tarehe: November 17th, 2024

Na. Faraja Msibe, DODOMA

CHAMA cha Alliance for African Farmers (AAFP) kimeridhishwa na mchakato wa uteuzi wa wagombea uliofanywa na wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuuita kuwa ulikuwa shirikishi.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Vijana wa Mkoa wa Dodoma wa Chama cha AAFP, Fredrick Mapua alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu mchakato wa uteuzi wa wagombea, mapingamizi na maamuzi ya rufaa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mapua alisema “nimekuja kuzungumzia mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuanzia uteuzi wa wagombea, mapingamizi na maamuzi ya rufaa. Nianze kwa kumshukuru sana Rais, mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya amejaribu sana kusimamia demokrasia nchini. Mchakato ulienda vizuri sana. Tulifanya vikao baina ya wasimamizi wa uchaguzi na vyama vya siasa kwa ajili ya kufanya uchaguzi kuwa huru na wa haki. Hivyo, mchakato ulikuwa shirikishi tangu awali. Kwa chama changu tulihudhuria vikao hivyo, nikiwepo mimi binafsi, tulikuwa tulipatiwa miongozo kila mjumbe nakala yake. Maelezo na kanuzi zilikuwa wazi. Wale wenye uwezo wa kusoma na kuandika walikuwa wanauwezo wa kusoma nakuelewa nini kilichokuwa kinahitajika na nini kilichokuwa hakihitajiki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Maelezo yalikuwa yanajitosheleza kwenye kanuni kama ulizifuata sidhani kama unaweza kuwa muanga wa wale walioenguliwa katika mchakato wa uchaguzi huu”.

Alisema kuwa kufuatia mchakato huo haki ilijaribu kutendeka na ilipatikana. Kwa wale walioona wameonewa fursa ya rufaa ilikuwepo. “Chama changu tulikaa na kujadili wapi tunamapungufu na wapi wenzetu wametuzidi ili tusionekane bado wadogo sana. Sisi tulifuata taratibu na kanuni zote. Hivyo, kwenye chama changu hakuna aliyeenguliwa kutokana na makosa madogo madogo kama walivyokuwa wakilalamika vyama tofauti kwenye mitandao ya kijamii. Kwa chama chetu wote tulikuwa makini na kulifuata maelekezo ya mwongozo” alisema Mapua.

Akiongelea amani na utulivu alisema kuwa ni wajibu wa vyama vya siasa. Alisema kuwa chama chake kimeweka mkakati kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu. “Sisi tunapenda amani, utulivu, siasa safi na salama. Hatupendi kuona watu wakiumia au kuharibikiwa mali kutokana na siasa. Ukiona mtu anatumia nguvu sana kutaka madaraka jiulize mara mbili” alisisitiza Mapua.

Katika hatua nyingine Katibu wa Chama cha Kijamii (CCK) Mkoa wa wa Dodoma, Abuutwahiru Iddi alisema kuwa mchakato wa kuteua wagombea ulifanyika vizuri ukiwa shirikishi. “Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa aliitisha vikao mbalimbali kwa lengo la kufanikisha zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. “CCK nayo ilishiriki kuhamasisha wananchi wake kuweza kuchukua fomu, zimejazwa na kurudishwa ofisi za serikali za mitaa kwa mujibu wa kalenda na ratiba. Mchakato umeenda vizuri na sasa tunajiandaa kufanya kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa tarehe 27 Novemba, 2024. Chama kinaendelea kuhamasisha wananchi ili kuelewa zaidi maana ya uchaguzi na waweze kujitokeza kupigia kura viongozi wanaowahitaji tofauti na kubaki nyumbani na wanapopatikana vongozi ambao hawawahitaji watabaki kulalamika kwa miaka mitano inayofuata” alisema Iddi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.