• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Chamwino, Mnadani, Tambukareli na Ipagala zaibuka kidedea Usafi

Imewekwa tarehe: May 10th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KATA za Chamwino, Mnadani, Tambukareli na Ipagala zimefanya vizuri zaidi katika ushiriki wa viongozi na wananchi kwenye mazoezi ya usafi wa Mazingira na upendezeshaji mji ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wa kulifanya jiji hilo kuwa usafi na la kuvutia kimazingira.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti wa taka ngumu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro katika Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kuwasilisha taarifa za utekelezaji za robo ya tatu (Januari-Machi, 2023) kutoka kwenye kata uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Kimaro alisema kuwa kuishi katika Mazingira safi na salama ni haki ya kisheria. “Sheria ya Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 kifungu cha 4 kinafafanua kuwa kila mtanzania ana haki ya kuishi katika Mazingira safi, salama na ya kiafya. Halmashauri imekuwa na juhudi kubwa za kuhamasisha wananchi wake kufanya usafi wa Mazingira, kupanda maua na miti katika maeneo yao ili kuhakikisha yanapendeza” alisema Kimaro.

Alisema kuwa kikao cha Kamati ya Mipango miji na Mazingira cha Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichoketi tarehe 25 Aprili, 2023 kilipendekeza kutoa vyeti vya pongezi kwa mitaa iliyofanya vizuri katika ushiriki wa viongozi na wananchi kwenye usafi wa Mazingira. “Mheshimiwa Mwenyekiti, mitaa iliyofanya vizuri ni Mwaja kutoka Kata ya Chamwino, Mtaa wa Karume kutoka Kata ya Mnadani, Mtaa wa Amani kutoka Kata ya Tambukareli na Mtaa wa Swaswa Halisia kutoka Kata ya Ipagala. Vigezo tulivyozingatia ni usafi wa mazingira kuzunguka nyumba, makazi na biashara, taasisi, mitaro ya maji ya mvua na maeneo ya wazi. Kikubwa zaidi ni ushawishi wa viongozi wa kisiasa hasa wenyeviti na mabalozi kushiriki kwenye usafi wa kaya na jumuiya” alisema Kimaro.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma inatekeleza mkakati wake wa kulifanya jiji hilo kuwa safi na lenye mandhari ya kupendeza kwa kuweka mkazo wa ushiriki wa wananchi katika kufanya usafi wa maeneo yao mita tano kuzunguka maeneo ya makazi na biashara.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.