• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Changamoto ya masoko yakwamisha juhudi zetu - Tunajikubali walemavu

Imewekwa tarehe: August 30th, 2021

KIKUNDI cha Tujikubali walemavu kinachoendesha kiwanda kidogo cha kutengeneza viatu vya ngozi kinakabiliwa na changamoto ya masoko jambo linalosababisha kusua kwa marejesho.

Kauli hiyo ilitolewa na Mweka Hazina wa kikundi hicho, Pauleta Lesso alipokuwa akisoma taarifa fupi ya kikundi hicho kwa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma ilipofanya ziara ya kukitembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na kikundi hicho Mtaa wa Nzuguni “B”.

Lesso alisema “kikundi chetu kinachojihusisha na kiwanda kidogo cha utengenezaji viatu vya ngozi kwa sasa shughuli zinaendelea vizuri, japo bado tuna changamoto ya masoko inayopelekea kusuasua kwa marejesho ya mkopo wetu”.   

Changamoto nyingine alizielezea kuwa ni miundombinu na usafiri wakati wa kutafuta masoko na kuuza bidhaa ni shida, alisema. “Changamoto nyingine ni kutawanyika kwa baadhi ya wanakikundi wenzetu kutokana na sababu zao binafsi na kupoteza uaminifu ndani ya kikundi” alisema Lesso.

Kuhusu mafanikio ya mradi, aliyataja kuwa wameweza kununua vifaa na malighafi kwa ajili ya kutengenezea viatu na kunufaika na mashine ambazo zilirahisisha kazi. “Mashine hizi ziliturahisishia kazi na kupelekea kupata fedha za marejesho na kujikimu kwa kila mwanakikundi. Hivyo, mkopo wa asilimia mbili ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya watu wenye ulemavu umeleta tija kwa walemavu. Watu wenye ulemavu wakishirikiana kwa pamoja huleta maendeleo chanya kwa kikundi, kila mwanakikundi na jamii kwa ujumla. Kupitia mkopo huu tumefanikiwa kujenga jengo dogo la ofisi yetu ambayo ipo kwenye hatua ya umaliziaji” alisema Lesso.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Dodoma, Meja Mst. Johnick Risasi aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuwawezesha watu wenye ulemavu kupata mikopo ya asilimia mbili kutoka mapato ya ndani. Alisema kuwa kitendo cha Halmashauri kuwakopesha watu wenye ulemavu ni kuonesha kuwajali watu hao. “Mheshimiwa Rais Samia anazungumzia usawa kwa watu wote. Watu wenye ulemavu wakiwezeshwa wanaweza kujiletea maendeleo. Ushauri, watu hawa watafutiwe sehemu nzuri na kuangalia jinsi ya kuwezeshwa kulipa pango. Huku wanapofanyia shughuli zao pamejificha sana” alisema Meja Mst. Risasi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Dodoma, Meja Mst. Johnick Risasi (aliyesimama) akitoa nasaha zake kwa wanakikundi cha Tunajikubali walemavu alipoambatana na kamati yake kutembelea miradi ya vikundi kutoka kwenye Kata za Jiji la Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.