• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Chanjo ya UVIKO-19 haina madhara kwa wajawazito - Dkt. Method

Imewekwa tarehe: August 7th, 2021

Na. Sifa Stanley, DODOMA

MGANGA Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method amewaondoa hofu wanawake wajawazito kuwa chanjo ya UVIKO-19 inayotolewa sasa nchini haina madhara kwao.

Hakikisho hilo alilitoa jana tarehe 6 Agosti, 2021 alipowasilisha mada juu ya tahadhari ya UVIKO-19 katika mkutano wa Baraza la Madiwani alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa viti maalum, Mhe. Khadija Shabani Taya (Keisha) aliyeuliza juu ya usalama wa chanjo ya UVIKO-19 kwa kina mama wajawazito hasa mfumo na ukuaji wa mimba.

Akijibu swali hilo, Mganga mkuu huyo alisema kuwa chanjo hizo ni salama kwa akina mama wajawazito. “Hakuna tafiti zinazoonesha chanjo inapelekea mimba kuharibika” alisema Dkt. Method.

Aidha, alisema kuwa chanjo ya UVIKO-19 kwa baadhi hupelekea maudhi madogo madogo ambayo hutofautiana kati ya mtu na mtu. maudhi hayo ni kama vile homa za usiku, mkono kuvimba, pamoja na kuchoka ambayo huisha ndani ya siku chache baada ya kupata chanjo na kuwaondoa hofu Madiwani akiwahakikishia kuwa chanjo ni salama. “Niwaondoe hofu Waheshimiwa Madiwani, chanjo ni salama, twende tukachanje” alisema Dkt. Method.

Akiongelea suala la umri sahihi wa mtoto kupatiwa chanjo, Mganga Mkuu alisema kuwa ugonjwa wa UVIKO-19 unaathiri makundi mbalimbali likiwemo kundi la watoto. Alisema kuwa watoto watakaopatiwa chanjo ni wale wenye umri wa miaka mitano na kuendelea. “Watoto wenye umri chini ya miaka mitano hawaathiriki sana na ugonjwa wa UVIKO-19” alisema Dkt. Method.

Aidha, Mganga Mkuu huyo alisema kuwa kwa hivi sasa serikali imeyapa kipaumbele makundi yaliyo katika hali hatarishi zaidi ya kupata maambukizi yaani watumishi wa afya, watu wenye umri wa zaidi ya miaka 50 na watu wenye magonjwa sugu.

Vile vile, aliweka wazi kuwa chanjo ya UVIKO-19 haina madhara kwa nguvu za kiume.

Akifafanua zaidi alisema kuwa chanjo haizuii kupata maambukizi ya UVIKO-19, bali wakichanja wengi katika jamii itazuia maambukizi yasiendelee kwenye jamii na inasaidia kupunguza makali ya virusi na vile vile mtu kutopata madhara makubwa ya kiafya endapo atapata maambukizi ya ugonjwa huo, alisema Mganga huyo.

Kuhusu uchukuaji wa tahadhari ya ugonjwa wa UVIKO-19, alishauri juu ya matumizi ya maji tiririka na sabuni au matumizi ya vitakasa mikono. Pia alishauri wananchi kupata chanjo ili kupunguza kasi ya maambukizi na vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.  

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.