• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Chongolo awapongeza wafanyakazi Kiwanda cha Mbolea Itracom

Imewekwa tarehe: June 26th, 2023

Na. Dennis Gondwe, NALA

KIWANDA cha Mbolea cha Itracom kimeajiri wafanyakazi 1,000 wengi wao katika maeneo ya uzalishaji na ujenzi na kusaidia katika kukabiliana na changamoto za ajira kwa vijana.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Mbolea cha Itracom, Nduwimana Nazaire alipokuwa akiwasilisha muhtasari wa kiwanda hicho kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, alipotembelea na kukagua kiwanda hicho katika Kata ya Nala.

Nazaire alisema “kiwanda kina jumla ya wafanyakazi wapatao 1,000. Kati ya hao 380 wana ajira za kudumu na wako moja kwa moja kwenye uzalishaji kiwandani. Idadi ilibaki wako katika Idara ya Ujenzi. Kwa wenye ajira za kudumu kuna watanzania 208 na warundi 172. Baada ya kumaliza usimikaji wa mitambo yote kiwanda, zitatolewa ajira kwa watanzania takribani 2,048 wa kada mbalimbali kufanya kazi kiwandani ili kufikia lengo la uzalishaji wa tani 1,000,000 za mbolea kwa mwaka. Kiwanda cha kuchanganya mbolea kitaajiri takriban watanzania 75. Mtambo wa kuzalisha chokaa utaajiri takribani warundi 10 na watanzania 54. Kiwanda cha kuchakata fosfeti mkoani Manyara, Vilima Vitatu kinachoendelea kujengwa kitaajiri takribani warundi 20 na watanzania 123 wanaofanya kazi katika kiwanda hicho ifikapo mwishoni mwa mwaka 2023. Hivyo, hadi kufikia mwisho wa mwaka 2023, kiwanda cha Intracom kitakuwa kimeajiri takribani wafanyakazi 3,067 (warundi 288 na watanzania 2,779).

Akiongelea faida za kiwanda, Mkurugenzi Mtendaji huyo alisema kuwa kiwanda kitakuwa kinazalisha bidhaa za mbolea na virekebishi vya udongo kiasi cha tani 1,500,000 kwa mwaka. Mbolea ya mseto ni 1,000,000, Chokaa Kilimo 300,000 na Mbolea mchanganyiko (blends) 200,000.

Faida nyingine ni wakulima wanapata mbolea kwa bei nafuu ukilinganisha na mbolea nyingine zinazouzwa nchini. Hivyo, kuwapunguzia mzigo wa gharama ya uzalishaji wa bidhaa za kilimo, aliongeza. “Chokaa Kilimo itakayotengenezwa itatumika pia kwa ajili ya kurekebisha tindikali ya udongo (Soil acidity). Hivyo, maeneo yenye udongo wenye tindikali nyingi hususani Nyanda za Juu Kusini na baadhi ya maeneo ya Kanda ya Ziwa yatafaidika na mbolea na virekebishi vya udongo. Samadi ya wanyama ambayo ni mojawapo ya malighafi muhimu sana katika uzalishaji wa mbolea zetu inanunuliwa kutoka kwa wafugaji wa Dodoma na baadae itatoka katika mikoa ya jirani na nchi nzima. Hii imetengeneza soko ili kuwapatia kipato na ajira wakulima na wafugaji wa ng'ombe wa vijijini nchini Tanzania” alisema Nazaire.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Daniel Chongolo aliwapongeza wafanyakazi wa kiwanda hicho. Aidha, aliwataka kufanya kazi kwa kujituma, uadilifu na uaminifu na kuwaasa wasijihusishe na vitendo vya udokozi. “Mjitume kutafuta tija ambayo inatakiwa kwa pande zote, kwa muwekezaji na kwetu sisio wafanyakazi. Huwa tunafikiri kinapoharibika, kinaharibika cha mwingine na sisi tunabaki salama. Lakini kikiharibika, sisi ndiyo wakwanza kupata madhara” alisema Chongolo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.