• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

CWT yakabidhi mifuko 300 ya saruji Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: October 4th, 2019

CHAMA cha walimu Tanzania (CWT) kimekabidhi mifuko 300 ya saruji yenye thamani ya shilingi 4,650,000 kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kuunga mkono ujenzi wa miundombini ya elimu ya msingi Jijini hapa.

Akikabidhi mifuko hiyo kwa Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma katika viunga vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania, Mwalimu Deus Seif alisema kuwa moto wa Chama cha Walimu ni Wajibu na Haki. Alisema kuwa Chama cha Walimu kinaamini ili mwalimu afundishe vizuri anahitaji mazingira mazuri ya kufundishia.

“Mwalimu akiingia darasani akakuta darasa zuri halina vumbi, lina sakafu, lina milango mizuri, lina madawati mazuri, Mwalimu atafanya kazi yake kwa raha na weledi. Lakini tunaamini mwalimu akiwa na nyumba nzuri ya kuishi tena karibu na eneo la kazi atafanya kazi nzuri zaidi. Vilevile tunaamini miundombinu ya vyoo si kwa walimu peke yake, hata kwa watoto kwa sababu rasilimali ya Mwalimu ni watoto kwa hiyo na watoto wakiwa katika mazingira yanayovutia kupokea kile anachotoa Mwalimu, Mwalimu atafanya kazi yake kwa amani sana” alisema Mwalim Seif.

Alisema kuwa madarasa yaliyopo katika Halmashauri ya Jiji ni asilimia 37.5, “kwa hiyo na sisi Mstahiki Meya tuwe sehemu ya kutatua changamoto hiyo” aliongeza Mwalim Seif. Mchango huo ni sehemu ya utaratibu wa chama hicho kurudisha shukrani katika jamii na umekuwa ukifanyika nchi nzima, aliongeza.  

Kwa upande wake, Afisa Elimu ya Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Joseph Mabeyo alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaupungufu wa vyumba vya madarasa 1,522, kati ya vyumba vya madarasa 916 vilivyopo, wakati mahitaji ni vyumba 2,438 vya madarasa. Akiongelea nyumba za walimu, alisema kuwa mahitaji ya nyumba za walimu ni 1,777, nyumba zilizopo ni 167 na kuifanya Halmashauri hiyo kuwa na upungufu wa nyumba 1,610. Kufuatia upungufu huo, Halmashauri iliamua kuwashirikisha wadau kuchangia ujenzi wa miundombinu hiyo.

Akipokea mifuko hiyo 300 ya saruji, Mstahiki Meya wa Jiji Dodoma Prof. Davis Mwamfupe alikishukuru Chama Cha Walimu kwa mwitikio wa kuchangia Sekta ya Elimu. Aidha, alitoa wito kwa vyama vya wafanyakazi na wadau wengine kuiga mfano wa Chama cha Walimu kuchangia sekta hiyo yenye mahitaji mengi. Katika kuonesha mfano, alichangia mifuko 10 ya saruji ili iwe hamasa kwa watu wengine katika kuboresha sekta hiyo.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina shule za msingi za serikali 93, zenye jumla ya wanafunzi 97,526.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.