• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dar yatoa mwongozo, utaratibu wa kuwapanga Machinga

Imewekwa tarehe: September 18th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla ametoa muda wa mwezi mmoja kwa madawati ya uwezeshaji wananchi kiuchumi yaliyopo katika kila Wilaya kuanza maandalizi ya kuwapanga upya na vizuri wafanyabiashara wadogo maarufu kama Machinga kuanzia Jumatatu Septemba 20, hadi Oktoba 18, 2021.

Makalla ametoa tamko hilo jana Septemba 17, 2021 wakati akizindua kitabu cha mpango wa kuwapanga vizuri wafanyabiashara hao Jijini Dar es Salaam.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema uwepo wa Machinga katika maeneo yasiyo umekuwa na athari nyingi ikiwemo kusababisha msongamano wa watu, ajali, kuikosesha Serikali mapato n ahata kukwamisha juhudi za mapambano dhidi ya ugonjwa wa Korona.

Akifafanua zaidi Makalla amesema mpango huo umewashirikisha wadau wote ikiwamo wafanyabiashara hao, jambo lililowezesha kujua kuwa wapo wafanyabiashara wangapi katika kila wilaya.

Aidha, aliyataja makundi matano ambayo mpango huo utawagusa kuwa ni wafanyabiashara waliojenga vibanda juu ya mifereji na mitaro, wale walio mbele ya maduka ya watu ambao husababisha wateja kushindwa kuingia na kutoka dukani.

Makundi mengine ni wafanyabiashara waliopo katika hifadhi za barabara, wanaofanya biashara na kuzuia njia za waenda kwa miguu, hali ambayo husababisha baadhi ya wapita njia kugongwa na magari kutokana na kulazimika kupita barabarani kabisa na pia wanaofanya biashara mbele ya taasisi za umma kama vile shule za msingi na sekondari, aliongeza Mhe. Makalla.

Vilevile, ameiagiza ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuendelea kuweka mabango ya katazo ya kufanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi.

Ameagiza pia kila Mkuu wa Wilaya kuhakikisha madawati ya uwezeshaji wananchi kiuchumi yanaratibu wamachinga hao bila bughudha.

Naye mwakilishi wa Wamachinga, Steven Lusinde ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Wamachinga Tanzania, amesema kuwa utaratibu huo wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ni mfano wa kuigwa kwa mikoa mingine nchini.

“Tumepokea agizo lako, tutalifikisha kwa wenzetu kama lilivyo ili kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Wakuu wa Wilaya. Tunaomba Wakuu wa Wilaya wazingatie hili kwamba kutupanga upya na kutupanga vizuri, kwa sababu kuna maeneo wanastalihi kutupanga vizuri maana tupo maeneo sahihi na si upya” alisema kiongozi huyo.

Lusinde alikiri kuwa ni kweli wamachinga wamekiuka utaratibu kwa kufanya biashara maeneo yasiyo rasmi.

“Niwaombe wanzangu popote walipo nikiwa kama Makamu Mwenyekiti wa Machinga Tanzania kwamba kwa maelekezo haya tuwe watulivu tuhakikishe tunajianga vizuri” alimalizia Lusinde.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.