• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Daraja la Hurui mkombozi kwa wananchi wa Kondoa na Babati

Imewekwa tarehe: August 23rd, 2024

Imeelezwa kuwa kujengwa kwa daraja la mto Hurui lenye urefu wa mita 30 lililopo katika kijiji cha Hurui kata ya Kikore wilayani Kondoa mkoani Dodoma limekuwa msaada mkubwa kwa wananchi waliokuwa wanapata adha ya muda mrefu ya usafiri kutokana na kukosekana kwa daraja baada ya daraja la awali kusombwa na maji ya mvua.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Dkt. Festo Dugange wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa daraja la Hurui wilayani Kondoa. Uwekaji wa jiwe la msingi umefanywa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango.

Amesema kama yalivyo maelekezo ya Mhe. Rais kuhakikisha vijiji vyote vinapitika kwa barabara, katika kipindi cha miaka mitatu (3) ya Rais Samia zaidi ya bilioni 7 na milioni 200 zimetolewa katika Wilaya ya Kondoa kwaajili ya  ujenzi wa barabara na madaraja. 

Pia ameongeza kuwa wao kama OR- TAMISEMI wamepokea maagizo ya Makamu wa Rais kuanza kujenga barabara ya 

Ntundwa-Hurui yenye urefu wa Km 46.8 ili wananchi waweze kuzifikia huduma za kijamii na waweze kufanya shughuli zao za kiuchumi wakati wote.

Vile vile Dkt. Dugange amempongeza Mhandisi Victor Seff kwa usimamizi mzuri wa fedha na ujenzi bora wa miundombinu ya barabara na madaraja za wilaya.

Naye Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Victor Seff amesema usanifu wa daraja umefanywa na wahandisi wa ndani chini ya Kitengo cha "TARURA Engineering and Environmental Consultanting Unit" na ujenzi umefanywa na Mkandarasi M/S Madata Investment Company Limited. Utekelezaji wake umefikia asilimia 95 kukamilika na daraja lina uwezo wa kubeba magari uzito wa tani 70 na litadumu kwa zaidi ya miaka 100.

"Daraja hili linaenda kuondoa changamoto ya mawasiliano kwa tarafa za Pahi na Bereko wilayani Kondoa pia  barabara inayotumika mpaka kufikia daraja hili inaunganisha barabara kuu kutoka Dodoma kwenda Babati", amesema.

Bw. Iddi Malatu mkazi wa kijiji cha Madege  Kata ya Kikole ameishukuru Serikali kwa kuwajengea daraja la mto Hurui kwani limewasaidia wananchi kusafiri na kusafirisha mazao yao na kuzifikia huduma za kijamii kwa urahisi.

"Daraja hili lilipoharibiwa na maji ya mvua tangu mwaka 2019 wananchi wa maeneo haya tulikuwa tukipata shida kuvuka kwenda ng'ambo ya pili kutokana na mto huu kujaa maji ambapo ilipelekea wanafunzi kushindwa kwenda shule pia hata wajawazito walikuwa wanajifungulia njiani kwa kushindwa kwenda zahanati iliyopo upande wa pili, kwakweli daraja hili ni mkombozi sana kwetu", alisema.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.