• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC anena, vijana wakubali kuchanja kwa hiari

Imewekwa tarehe: August 5th, 2021

Na Sifa Stanley na Getruda Shomi

VIJANA wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wajitokeza kupata chanjo ya UVIKO-19 katika kituo cha Afya Makole ikiwa ni mwitikio wao baada ya kuhamasishwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri.

Vijana hao 30 walionesha mwitikio huo baada ya kuhamasishwa juu ya chanjo na usalama wake na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipofanya ziara na kuzungumza na wafanyabiashara wa soko la Sabasaba jijini hapa.

Shekimweri aliwahakikishia usalama wa chanjo hiyo na kuwaeleza kwamba hata yeye ameshapata chanjo. Aliwataka wananchi kuondoa hofu na kujitokeza kwa wingi kupata chanjo ambayo inatolewa bure na kwa hiari.

Mkuu wa Wilaya alivitaja vituo vinavyotoa chanjo ya UVIKO-19 katika Wilaya ya Dodoma kuwa ni Kituo cha Afya Makole, Kituo cha Afya Hombolo, Hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa, Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma (General), Hospitali ya St. Gema, Hospitali ya Chuo Kikuu cha Dodoma na Hospitali ya DCMC. “Mimi jana nimechanja, sijapata kadhia yoyote, nimeshinda salama, nimelala salama, na kazi inaendelea” alisema Shekimweri.

Aidha, aliwataka wakazi wa Jiji la Dodoma kupuuza taarifa za upotoshaji katika mitandao ya kijamii na kufuata taarifa na maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya. Baadhi ya mitandao inatoa taarifa zisizo sahihi na za kupotosha kwa sababu watu wengi hujifanya wataalamu wa afya, aliongeza.

Mkuu huyo wa wilaya aliwataka wafanyabiashara kuzingatia kanuni za kujikinga na UVIKO-19 kwa kuhakikisha maji tiririka na sabuni yanakuwepo katika maeneo yao ya biashara. Alisema kuwa iwapo maji tiririka na sabuni havitakuwepo katika maeneo ya biashara watazuiliwa kufanya biashara zao. “Kufikia kesho ikiwa hakuna maji tiririka, sabuni na vitakasa mikono, tutawazuia shughuli hizo kwa lengo la kuokoa maisha yenu na wananchi wengine” alisisitiza Shekimweri.

Wakati huohuo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma aliwataka askari wa usalama barabarani kusimamia sheria ikiwemo daladala kutokusimamisha abiria ili wawe sehemu ya mapambano ya UVIKO-19.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.