• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC azindua kituo cha kukusanyia mifuko ya plastiki

Imewekwa tarehe: May 31st, 2019

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Patrobas Katambi ameagiza apatiwe orodha ya majina ya taasisi zote katika Wilaya hiyo zinazokaidi kulipa tozo ya uzoaji taka kwa ajili ya usafi wa mazingira hali inayopelekea kuhatarisha afya za wakazi wa Jiji.

Katambi aliyeongozana na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi, alitoa kauli hiyo alipokuwa akizindua kituo cha kupokelea mifuko ya plastiki katika Kata ya Uhuru leo asubuhi.

"Tuna wajibu wa kuhakikisha mazingira yanakuwa salama, zipo taasisi ambazo hazilipi tozo ya uzoaji taka...naomba orodha ya majina ya taasisi zote zinazokaidi kulipia tozo ya taka kwani haiwezekani uchafue wewe mazingira, kisha kipindupindu tuugue sisi” alisema. 

Vilevile, aliwataka watendaji kuwasimamia wananchi katika maeneo yao ili kuhakikisha mazingira yao yanakuwa safi na kwa wanaokaidi kufanya usafi katika maeneo yao au kulipa tozo za kuzolea taka orodha yao iwasilishwe kwake.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema “agenda ya mifuko ya plastiki ni sehemu ya agenda yetu, vyombo vyote vichukue hatua kali bila kumvumilia mtu kwani mifuko ya plastiki imekuwa na athari kubwa katika mazingira ikiwemo kuziba mifereji ya maji na kusababisha uchafu kuzagaa na mafuriko na kusababisha vifo kwa mifugo pindi wanapokula mifuko hiyo" alisema.

Awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alisema kuwa jiji lake litaongoza katika kampeni ya upigaji marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki. “Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, jiji la Dodoma tunaenda kuongoza na kuwa wa mfano Tanzania. Tumekuwa na utamaduni wa kuongoza katika mapato, usafi, afya, elimu, sababu kubwa sisi wote ni vijana. Tunafikiria miaka 50 ijayo ya siyo miaka 50 iliyopita” alisema Kunambi. Aidha, aliwapongeza wakazi wa jiji la Dodoma kwa utulivu na ushirikiano wanaoendelea kumpatia katika kutekeleza majukumu yake.

Kunambi aliwataka wakazi wa jiji hilo kutii sheria bila shuruti na kusema kuwa usafi wa mazingira ni jukumu la kila mtu. Katika nyumba yako au eneo unalofanyia shughuli zako, hakikisha hakuna mfuko wa plastiki unaozagaa, atakayekutwa atachukuliwa hatua za kisheria, aliongeza.

Mkurugenzi wa jiji alieleza masikitiko yake kwa baadhi ya taasisi zinazokwamisha juhudi za usafi wa mazingira kwa kukataa kulipa tozo za uzoaji taka katika maeneo yao. “Wengine wanafikiria usafi siyo sehemu yao. Zipo taasisi kubwa hazilipi tozo ya usafi wa mazingira. Tusimame pamoja ili kusafirsha jiji letu” aliongeza Kunambi.

Nae mkuu wa idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu katika Halmashauri ya jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa Halmashauri hiyo ilijikita katika kutoa elimu kuanzia ngazi ya mtaa, kata na wilaya juu ya katazo la serikali la matumizi ya mifuko ya plastiki na kuelezea mifuko mbadala. Alisema kuwa elimu hiyo ilitolewa kwa njia ya redio, televisheni, magazeti, mitandao ya kijamii, matangazo mbalimbali na kupitia taasisi kama shule na maeneo ya masoko ili kuhakikisha elimu hiyo inawafikia wananchi wengi.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.