• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC, Mkurugenzi wamaliza migogoro ya Ardhi

Imewekwa tarehe: May 4th, 2019

MKUU wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Godwin Kunambi kwa pamoja wamemaliza na kuhitimisha migogoro ya Ardhi ya muda mrefu katika Kata mbili za Kikuyu Kusini na Kikuyu Kaskazini Jijini Dodoma ambapo wananchi wote waliothibitika kuhusika na maeneo yaliyokuwa na migogoro watapatiwa viwanja mbadala na vya bei nafuu vilivyopimwa na Jiji hilo kwa ajili ya makazi.

Baada ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kufanya uchunguzi wa kina kuhusu mgogoro huo, wakazi wapatao 233 katika Kata ya Kikuyu Kusini watapatiwa viwanja mbadala na wakazi 458 wa Kata ya Kikuyu Kaskazini waliothibitika kuvamia eneo lililokuwa la msitu watapatiwa viwanja vya bei nafuu, huku wakazi wapatao 15 wa Kata hiyo wakipatiwa viwanja mbadala bure.

Wakazi hao wanadaiwa kuvamia maeneo yaliyokuwa yamehifadhiwa yakiwemo ya misitu na barabara na kuanzisha makazi na shughuli za kiuchumi kwa miaka kadhaa, lakini Halmashauri ya Jiji hilo imeamua kuwapa viwanja vilivyopimwa kama sehemu ya kuwasaidia wakazi wake na kumaliza kabisa migogoro ya ardhi katika Kata hizo.

Viongozi hao kwa pamoja walifanya mikutano ya hadhara katika Kata hizo jana Aprili 2, 2019 na kuzungumza na wakazi wa Kata hizo, ambao walikuwa na malalamiko ya kuondolewa katika maeneo wanayodaiwa kuvamia kinyume na sheria.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji Kunambi aliwashauri wakazi hao kutouza viwanja wanavyopewa kama fidia badala yake waviendeleze kwani baada ya kila muhusika kupewa kiwanja chake, Halmashauri haitegemei kusikia mgogoro wowote au madai yanayohusiana na viwanja kutoka kwenye maeneo hayo.

“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya pamoja na wananchi, baada ya zoezi la kuwapa viwanja mbadala wahusika hawa, sitegemei kusikia mgogoro tena katika Kata hii, suala hili leo tunalifunga rasmi…nawashauri msiuze viwanja vyenu tutakavyowapa bali mviendeleze kwa manufaa yenu na watoto wenu” alisema Kunambi.

Kunambi alisema Halmashauri imetenga takribani viwanja 5,000 vyenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 7 kwa ajili ya kuvitoa bure kama fidia kwa wananchi kwa maeneo yenye migogoro sugu ya Ardhi Jijini humo, na kwamba mpango huo ndiyo suluhisho la migogoro yote ya Ardhi katika Halmashauri hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Katambi aliwatahadharisha wakazi wa Wilaya hiyo kuacha tabia ya kuhamasishana kuvunja sheria kwa vigezo vya kudai haki vinginevyo wafuate taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa Sheria za Nchi.

Akizungumza na wakazi wa Kata hizo, Katambi alisema kumekuwa na baadhi ya watu wanaoshawishi wenzao kuvunja sheria na kuvuruga amani bila sababu ya msingi na kwamba Serikali haitawavumilia endapo hawataacha tabia hiyo.

Alisema awali alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mwaka 2018, alifanya ziara katika Kata hizo mbili za Kikuyu Kusini na Kaskazini Mwezi Septemba ambapo alimuagiza Mkurugenzi wa Jiji kupeleka timu ya wataalam wa Ardhi ili wafanye uchunguzi wa kina wa migogoro iliyopo ili kupata ufumbuzi.  

“Ripoti ya kina kuhusu mgogoro wa hapa Kikuyu Kusini imekamilika na Mkurugenzi ameshanikabidhi hii hapa mikononi mwangu, inaeleza kila kitu…nyinyi wote mlivamia eneo la Serikali na hakuna hata mmoja mwenye nyaraka za umiliki za eneo hilo…Mkurugenzi anafanya hisani tu kuwapa viwanja mbadala kwa sababu Serikali ya awamu ya tano inajali wananchi wanyonge” alisema Katambi huku akiwaonesha wakazi hao ripoti ya uchunguzi wa mgogoro huo. 

Mkuu huyo wa Wilaya aliwaeleza wakazi hao kuwa, Mkurugenzi wa Jiji na wataalam wake wa Ardhi wamefanya kazi nzuri katika hatua zote za kuchunguza mgogoro huo kwani ripoti imeainisha kila kipande cha Ardhi kinacholalamikiwa na mmiliki wake amepigwa picha kama sehemu ya vielelezo vya msingi.

Viongozi hao wa Wilaya ya Dodoma wako katika ziara ya kutembelea maeneo yenye migogoro ya Ardhi ili kuhakikisha inamalizika kabisa katika Jiji la hilo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.