• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC Shekimweri ahimiza mpango wa lishe bora shuleni

Imewekwa tarehe: January 7th, 2025

Na. Aisha Ibrahim, DODOMA

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri aliwataka wakuu wa shule na walimu wakuu kutekeleza mpango wa huduma ya chakula kwa wanafunzi wote shuleni ili kuhakikisha wanapata lishe bora jambo litakalopelekea kujifunza kwa ufanisi.

Aliyasema hayo ofisini kwake wakati akihamasisha wazazi na walezi kujitokeza kwa wingi kuandikisha watoto shuleni katika ngazi ya awali na msingi pia wale wanaojiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2025.

Akisisitiza kuhusu mpango wa huduma ya chakula kwa wanafunzi shuleni, “……kuna uhusiano mkubwa sana kati ya ufaulu na lishe, mtoto ambaye hajashiba ni ngumu sana kumsikiliza mwalimu akamuelewa na akazingatia, ni tofauti na mtoto aliyepata chakula shuleni” alisema Alhaj Shekimweri.

Kwa upande wa wazazi na walezi katika Jiji la Dodoma walisema kuwa wamepokea vizuri mpango wa huduma ya chakula kwa wanafunzi shuleni ili kuhakikisha wanapata lishe bora ikiwa ni chachu ya maendeleo ya wanafunzi kiujumla.

Charles Maganya, mzazi kutoka Kata ya Ihumwa alisema kuwa mpango huo kama utatekelezwa vizuri utasaidia katika maendeleo ya watoto wawapo shuleni kwa sababu ili mtoto ajifunze ni lazima awe ameshiba na kuwa imara kimwili na kiakili. “Ni mpango mzuri na umepokelewa vizuri. Mpango huu kwa namna moja utakuwa ni chachu kubwa ya maendeleo ya watoto wetu shuleni kwa sababu watapata nafasi ya kusoma bila shida wakiwa wameshiba” alisema Maganya.

Akiongelea kuhusu kuhakikisha wanafunzi wanapata lishe bora shuleni, mkazi wa Kata ya Ipagala, Bathseba Njigo, alifafanua kuwa wao kama wazazi wanahakikisha wanaunga mkono jitihada hizo kwa kuchangia vyakula shuleni ili kuhakikisha watoto wanakaa darasani wakiwa wameshiba tayari kwa kupokea kile wanachofundishwa na walimu. “Uzuri ni kwamba shule nyingi zina utaratibu wa kuchangia chakula, sisi kama wazazi kwa nafasi yetu sehemu kubwa tunajitahidi kuunga mkono hizo jitihada ili watoto waweze kukaa darasani wakiwa wameshiba, waweze kupokea kile walimu wanachowapatia” alisema Njigo.

Aliongeza kuwa kuna baadhi ya wazazi hupuuzia jambo hilo wakidhania kuwa ni michango isiyokuwa na ulazima. Alisema kuwa wazazi hao hawawatendei haki watoto wao na wadau wengine wa elimu wanaoweka jitihada katika kuboresha elimu, ufaulu wa wanafunzi na taifa kwa ujumla.

Nae, mkazi wa Kata ya Ihumwa, Esther Yohana, aliwashauri wazazi na walezi kujitoa ipasavyo katika kuchangia vyakula na michango mingine kwa wanafunzi ili kuimarisha mpango wa lishe bora shuleni kwa sababu ni faida kwa wanafunzi, wazazi na taifa kwa ujumla. “Wazazi tuchangie kwa sababu ni faida watoto wetu na kwa taifa letu” alisema Yohana.

Wazazi, walimu na wadau wote wa elimu nchini wanatakiwa kushirikiana ipasavyo katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mahitaji muhimu shuleni ikiwemo elimu bora na lishe bora ili kuimarisha afya zao kimwili na kiakili kwa lengo la kutengeneza nguvu kazi ya taifa imara.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.