• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC. Shekimweri alipongeza Jiji la Dodoma kwa kuanzisha Kliniki ya Ardhi

Imewekwa tarehe: October 17th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepongezwa kwa kuanzisha Kliniki ya Ardhi iliyowafanya wataalam kutoka ofisini na kuweka kambi kuwahudumia wananchi eneo moja ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo eneo la Manispaa ya zamani alipotembelea na kukagua maendeleo ya Kliniki ya Ardhi inayotoa huduma jijini hapa.

Shekimweri alisema “kipekee nimpongeze Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, niliyasema haya wakati tunakupokea hapa Dodoma baada ya kuteuliwa. Mimi nakufahamu unavyofanya kazi. Ninafahamu ni mtu unaejali sana watu na matatizo ya wananchi. Nilikuwa nawaambia wananchi ninajua kuna mkurugenzi atawasilikiza kwa nafasi na kwa staa na atawashughulikia matatizo yenu yaliyowasumbua kwa muda mrefu”.

Alisema kuwa Rais alishaelekeza wataalam kutoka ofisini na kwenda kwa wananchi kutatua kero zao. “Haya ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais kwamba tutoke ofisini na kwenda kushughulikia matatizo ya wananchi. Na hapa Dodoma sekta ya Ardhi ndiyo kero sugu. Tatizo kubwa lazima lishughulikiwe kwa ukubwa wake. Nimekuja hapa kukupongeza na kukutia nguvu pamoja na menejimenti, lakini kupongeza utaratibu huu. Hapa wataalam wote wapo hivyo hakuna kupigana tarehe” alisema Shekimweri.

Mkuu huyo wa wilaya aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika kliniki hiyo. “Niwapongeze wananchi wote mliojitokeza kwa wingi siku ya leo. Jana wananchi zaidi ya 1,000 walijitokeza hii inaonesha mlivyo na imani na serikali yenu katika kutatua kero zenu. Niwaombe kuendelea kutuamini tuna dhamira ya dhati kushughulikia matatizo yenu” alisema Shekimweri.

Akiwa katika kliniki hiyo Mkuu wa Wilaya ya Dodoma pamoja na mambo mengine alikabidhi hati miliki saba kwa wananchi zilizoandaliwa muda mfupi uliopita.

Kwa upande wake mwananchi wa Dodoma mjini, Mwajuma Seja alimshukuru Mungu kwa kupata hati yake. “Mheshimiwa Mkuu wa wilaya na mkurugenzi wa jiji pia nawashukuru sana kupata hati yangu. Sipo peke yangu wapo wenzengu 24, mimi peke yangu ndio nimebahatika kupata Hati wenzangu wote hawajapata hata ‘control number’ alisema Seja kwa masikitiko.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.