• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dc Shekimweri apokea madarasa 29 ya UVIKO-19

Imewekwa tarehe: December 23rd, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WILAYA ya Dodoma imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kiasi cha shilingi 580,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 29 ya shule za sekondari ili kuwawezesha wanafunzi wa kidato cha kwanza kusoma katika mazingira bora na salama.

Shukrani hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipokabidhiwa madarasa 29, ofisi 24 na viti na meza 1,450 katika shule ya sekondari Ng’hoghona iliyopo jijini Dodoma.

Shekimweri alisema “tunamshukuru sana Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwanza siyo tu kwa fedha alizozitoa lakini kwa kufikiria kizalendo namna sahihi ya matumizi ya fedha za Uviko-19 na kuweka tofauti na viongozi wengine karibia wote wa Afrika. Fedha za Uviko -19 zimetolewa na Benki ya Dunia kama mchango wao kwenye mapambano ya Uviko-19. Maono ya Rais wetu na dhamira njema siyo tu kuwa na matumizi ya mara moja lakini uendelevu wa kushughulika na changamoto. Alijihoji na kutusaidia kutupatia dira kushughulika na jambo hili. Ikiwa Uviko-19 inatokana na msongamano kumbe namna ya kushughulika na Uviko-19 pamoja na kunawa maji ni kuondoa msongamano”.

Mkuu huyo wa wilaya aliridhishwa na matumizi ya fedha na kusema kuwa fedha hiyo imetumika kwa maeneo yaliyokusudiwa na kuona fahari kwa kazi iliyofanyika. “Namna ya kumuunga mkono Mheshimiwa Rais, namna ya kumtia nguvu na namna ya kuomba maeneo mengine atuangalie pamoja na kushukuru kwa kiwango cha juu cha kushukuru. Sisi tunashukuru sana ametusaidia parefu sana tumesikia taarifa ya Mkurugenzi wa Jiji kuwa maoteo yetu ni kusajili watoto 12,151” alisema Shekimweri.

Akitoa taarifa ya makabidhiano ya madarasa 29, ofisi 24 na meza na viti 1,450 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inatarajia kupokea wanafunzi 12,151 watakaojiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023. “Idadi hii ya wanafunzi ni nyongeza ya wanafunzi 3,140 ukilinganisha na wanafunzi waliojiunga kidato cha kwanza mwaka 2022. Kufuatia upungufu uliokuwepo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilipokea kiasi cha shilingi 580,000,000 katika shule 23 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 29” alisema Mafuru.

Alisema kuwa halmashauri yake ilitekeleza mradi huo kwa njia ya “force account” ambapo wakuu wa shule walikasimishwa madaraka ya usimamizi wa mradi huo. “Mradi ulianza tarehe 10 Oktoba, 2022 kwa shule zote 23 na usimamizi na ufuatiliaji ulifanywa na ofisi ya Mhandisi wa Jiji na wataalam wengine pamoja na ufuatiliaji wa karibu wa Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Dodoma na wadaun wengine. Kufukia tarehe 30 Novemba, 2022 ujenzi huo ulikamilika kwa shule zote 23 ambapo madarasa 29 yalijengwa, ofisi za walimu 24 pamoja na meza na viti 1,450 kwa wastani wa meza na viti 50 kwa kila darasa” alisema Mafuru.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.